< Mwanzo 15 >

1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
After - the things these it came [the] word of Yahweh to Abram in the vision saying may not you fear O Abram I [am] a shield of you reward your [will be] great very.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
And he said Abram O Lord Yahweh what? will you give to me and I [am] going childless and [the] son of [the] acquisition of household my he [is] Damascus Eliezer.
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
And he said Abram here! to me not you have given offspring and there! [the] son of household my [is] inheriting me.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
And there! [the] word of Yahweh [was] to him saying not he will inherit you this [one] that except [one] who he will come out from inward parts your he he will inherit you.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
And he brought out him the outside towards and he said look please the heavens towards and count the stars if you are able to count them and he said to him thus it will be offspring your.
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
And he believed in Yahweh and he credited it to him righteousness.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
And he said to him I [am] Yahweh who I brought out you from Ur of [the] Chaldeans to give to you the land this to take possession of it.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
And he said O Lord Yahweh how? will I know that I will take possession of it.
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
And he said to him bring! to me a heifer three years old and a goat three years old and a ram three years old and a turtle-dove and a young pigeon.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
And he brought to him all these and he cut in pieces them in the middle and he set each piece its to meet neighbor its and the bird[s] not he cut in two.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
And it came down the bird[s] of prey on the carcasses and he drove away them Abram.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
And it was the sun [about] to go and a deep sleep it fell on Abram and there! dread darkness great [was] falling on him.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
And he said to Abram certainly you will know that a sojourner - it will be offspring your in a land [which] not [belongs] to them and they will serve them and they will afflict them four hundred year[s].
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
And also the nation which they will serve [will be] judging I and after thus they will come out with possession[s] great.
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
And you you will go to ancestors your in peace you will be buried in old age good.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
And [the] generation fourth they will return hither for not [is] complete [the] iniquity of the Amorite[s] until now.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
And it was the sun it had gone and darkness it was and there! a fire pot of smoke and a torch of fire which it passed between the pieces these.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
On the day that he made Yahweh with Abram a covenant saying to offspring your I give the land this from [the] river of Egypt to the river great [the] river of Euphrates.
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
The Kenite[s] and the Kenizzite[s] and the Kadmonite[s].
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
And the Hittite[s] and the Perizzite[s] and the Rephaites.
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
And the Amorite[s] and the Canaanite[s] and the Girgashite[s] and the Jebusite[s].

< Mwanzo 15 >