< Mwanzo 15 >
1 Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
After these things the word of Jehovah came to Abram in a vision, saying, Fear not, Abram; I am thy shield, thy exceeding great reward.
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina hata mtoto na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
And Abram said, Lord Jehovah, what wilt thou give me? seeing I go childless, and the steward of my house is this Eliezer of Damascus.
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
And Abram said, Lo, to me thou hast given no seed, and behold, a son of my house will be mine heir.
4 Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.”
And behold, the word of Jehovah [came] to him, saying, This shall not be thine heir, but he that will come forth out of thy body shall be thine heir.
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu kuelekea mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
And he led him out, and said, Look now toward the heavens, and number the stars, if thou be able to number them. And he said to him, So shall thy seed be!
6 Abramu akamwamini Bwana, naye kwake hili likahesabiwa kuwa haki.
And he believed Jehovah; and he reckoned it to him [as] righteousness.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Bwana, niliyekutoa toka Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
And he said to him, I am Jehovah who brought thee out of Ur of the Chaldeans, to give thee this land to possess it.
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitapata kuimiliki?”
And he said, Lord Jehovah, how shall I know that I shall possess it?
9 Ndipo Bwana akamwambia, “Niletee mtamba wa ngʼombe, mbuzi na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
And he said to him, Take me a heifer of three years old, and a she-goat of three years old, and a ram of three years old, and a turtle-dove, and a young pigeon.
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege, hakuwapasua vipande viwili.
And he took all these, and divided them in the midst, and laid the half of each opposite its fellow; but the birds he did not divide.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
And the birds of prey came down on the carcases; and Abram scared them away.
12 Wakati jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, giza nene na la kutisha likaja juu yake.
And as the sun was just going down, a deep sleep fell upon Abram; and behold, a horror, a great darkness, fell upon him.
13 Kisha Bwana akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni kwenye nchi ambayo si yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
And he said to Abram, Know assuredly that thy seed will be a sojourner in a land [that is] not theirs, and they shall serve them; and they shall afflict them four hundred years.
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
But also that nation which they shall serve I will judge; and afterwards they shall come out with great property.
15 Wewe, hata hivyo utakwenda kwa baba zako kwa amani na kuzikwa katika uzee mwema.
And thou shalt go to thy fathers in peace; thou shalt be buried in a good old age.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana dhambi ya Waamori bado haijafikia kipimo kilichojaa.”
And [in the] fourth generation they shall come hither again; for the iniquity of the Amorites is not yet full.
17 Wakati jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
And it came to pass when the sun had gone down, and it was dark, that behold, there was a smoking furnace, and a flame of fire which passed between those pieces.
18 Siku hiyo Bwana akafanya Agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati,
On the same day Jehovah made a covenant with Abram, saying, Unto thy seed I give this land, from the river of Egypt to the great river, the river Euphrates;
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
the Kenites, and the Kenizzites, and the Kadmonites,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
and the Hittites, and the Perizzites, and the Rephaim,
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
and the Amorites, and the Canaanites, and the Girgashites, and the Jebusites.