< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
Or il arriva en ce temps-là qu’Amraphel roi de Sennaar, Arioch roi de Pont, Chodorlahomor roi des Elamites, et Thadal roi des Nations
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
Firent la guerre à Bara roi de Sodome, à Bersa roi de Gomorrhe, à Sennaab roi d’Adama, à Séméber roi de Séboïm et au roi de Bala, la même que Ségor.
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
Tous ces rois s’assemblèrent dans la vallée des Bois, qui est maintenant la mer de sel.
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Car pendant douze ans ils avaient été soumis à Chodorlahomor, et à la treizième année ils s’étaient séparés de lui.
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
C’est pourquoi à la quatorzième année, Chodorlahomor vint, et les rois qui étaient avec lui; et ils battirent les Raphaïtes et les Zuzites à Astarothcarnaïm, et les Emites à Savé Cariathaïm,
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
Et les Chorréens dans les montagnes de Séir jusqu’à la plaine de Pharan, qui est dans le désert.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
Puis ils retournèrent et vinrent à la fontaine de Misphat, le même lieu que Cadès; et ils ravagèrent toute la contrée des Amalécites et des Amorrhéens qui habitaient à Asasonthamar.
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
Alors partirent le roi de Sodome, le roi de Gomorrhe, le roi d’Adama, le roi de Séboïm et le roi de Bala, la même que Ségor: et ils rangèrent leur armée en bataille contre eux, dans la vallée des Bois;
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
C’est-à-dire, contre Chodorlahomor roi des Elamites, Thadal roi des Nations, Amraphel roi de Sennaar et Arioch roi de Pont: quatre rois contre cinq.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
Or la vallée des Bois avait beaucoup de puits de bitume. C’est pourquoi les rois de Sodome et de Gomorrhe, ayant pris la fuite, y tombèrent, et ceux qui étaient restés s’enfuirent sur la montagne.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
Et ils enlevèrent toutes les richesses de Sodome et de Gomorrhe et tous les vivres, et ils s’en allèrent.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
Ils enlevèrent aussi avec toutes ses richesses Lot, fils du frère d’Abram, qui habitait à Sodome.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
Et voilà qu’un homme qui s’était sauvé annonça cette nouvelle à Abram qui habitait dans la vallée de Mambré l’Amorrhéen. frère d’Escol, et frère d’Aner; car ceux-ci avaient fait alliance avec Abram.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
Quand Abram eut entendu cela, c’est-à-dire que Lot son frère était captif, il prit les plus agiles de ses serviteurs, nés dans sa maison, au nombre de trois cent dix-huit, et poursuivit les ennemis jusqu’à Dan.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
Puis, ses alliés divisés, il fondit sur eux pendant la nuit, les battit et les poursuivit jusqu’à Hoba, qui est à la gauche de Damas.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
Il reprit toutes les richesses, et Lot son frère avec ses richesses, de même que les femmes et le peuple.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
Mais le roi de Sodome sortit au-devant de lui, lorsqu’il revenait après la défaite de Chodorlahomor, et des rois qui étaient avec lui dans la vallée de Savé, qui est la vallée du roi.
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
Mais Melchisédech roi de Salem, offrant du pain et du vin. car il était prêtre du Dieu très haut,
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
Le bénit, et dit: Béni soit Abram par le Dieu très haut, qui a créé le ciel et la terre;
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
Et béni le Dieu très haut, qui te protégeant, les ennemis ont été livrés entre tes mains! Et Abram lui donna la dîme de tout.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
Mais le roi de Sodome dit à Abram: Donne-moi les âmes, et prends le reste pour toi.
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
Abram lui répondit: Je lève ma main vers le Seigneur Dieu très-haut, possesseur du ciel et de la terre,
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
Que depuis le fil de la trame jusqu’à la courroie d’une chaussure, je ne recevrai rien de tout ce qui est à toi, afin que tu ne dises pas: J’ai enrichi Abram.
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
J’excepte seulement ce que mes jeunes gens ont mangé, et les parts des hommes qui sont venus avec moi, Aner, Escol, et Mambré: ceux-ci recevront leurs parts.

< Mwanzo 14 >