< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
and to be in/on/with day Amraphel king Shinar Arioch king Ellasar Chedorlaomer king Elam and Tidal king Goiim
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
to make battle with Bera king Sodom and with Birsha king Gomorrah Shinab king Admah and Shemeber king (Zeboiim *Q(k)*) and king Bela he/she/it Zoar
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
all these to unite to(wards) Valley (of Siddim) [the] Valley he/she/it sea [the] Salt (Sea)
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
two ten year to serve [obj] Chedorlaomer and three ten year to rebel
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
and in/on/with four ten year to come (in): come Chedorlaomer and [the] king which with him and to smite [obj] Rephaim in/on/with Ashteroth-karnaim Ashteroth-karnaim and [obj] [the] Zuzim in/on/with Ham and [obj] [the] Emim in/on/with Shaveh Kiriathaim
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
and [obj] [the] Horite in/on/with mountain: hill country their Seir till El-paran El-paran which upon [the] wilderness
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
and to return: return and to come (in): come to(wards) En-mishpat En-mishpat he/she/it Kadesh and to smite [obj] all land: country [the] Amalekite and also [obj] [the] Amorite [the] to dwell in/on/with Hazazon-tamar Hazazon-tamar
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
and to come out: come king Sodom and king Gomorrah and king Admah and king (Zeboiim *Q(k)*) and king Bela he/she/it Zoar and to arrange with them battle in/on/with Valley (of Siddim) [the] Valley
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
with Chedorlaomer king Elam and Tidal king Goiim and Amraphel king Shinar and Arioch king Ellasar four king with [the] five
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
and Valley (of Siddim) [the] Valley well well bitumen and to flee king Sodom and Gomorrah and to fall: fall there [to] and [the] to remain mountain: hill country [to] to flee
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
and to take: take [obj] all property Sodom and Gomorrah and [obj] all food their and to go: journey
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
and to take: take [obj] Lot and [obj] property his son: child brother: male-sibling Abram and to go: journey and he/she/it to dwell in/on/with Sodom
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
and to come (in): come [the] survivor and to tell to/for Abram [the] Hebrew and he/she/it to dwell in/on/with terebinth Mamre [the] Amorite brother: male-sibling Eshcol and brother: male-sibling Aner and they(masc.) master: men covenant Abram
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
and to hear: hear Abram for to take captive brother: male-relative his and to empty [obj] trained his born house: household his eight ten and three hundred and to pursue till Dan
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
and to divide upon them night he/she/it and servant/slave his and to smite them and to pursue them till Hobah which from left: north to/for Damascus
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
and to return: return [obj] all [the] property and also [obj] Lot brother: male-relative his and property his to return: return and also [obj] [the] woman and [obj] [the] people
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
and to come out: come King's Sodom to/for to encounter: meet him after to return: return he from to smite [obj] (Chedorlaomer *LBH(A)*) and [obj] [the] King's which with him to(wards) Valley (of Kings) Shaveh he/she/it Valley (of Kings) [the] King's
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
and Melchizedek Melchizedek king Salem to come out: send food: bread and wine and he/she/it priest to/for El (Most High) (LORD) Most High
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
and to bless him and to say to bless Abram to/for El (Most High) (LORD) Most High to buy heaven and land: country/planet
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
and to bless El (Most High) (LORD) Most High which to deliver enemy your in/on/with hand: power your and to give: give to/for him tithe from all
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
and to say king Sodom to(wards) Abram to give: give to/for me [the] soul: person and [the] property to take: take to/for you
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
and to say Abram to(wards) king Sodom to exalt hand my to(wards) LORD El (Most High) (LORD) Most High to buy heaven and land: country/planet
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
if: surely no from thread and till thong sandal and if: surely no to take: take from all which to/for you and not to say I to enrich [obj] Abram
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
beside me except which to eat [the] youth and portion [the] human which to go: went with me Aner Eshcol and Mamre they(masc.) to take: take portion their

< Mwanzo 14 >