< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
And it came to pass, in the day of Amraphel king of Shinar, Arioch king of Ellasar, Kedorlaomer king of Elam, and Tidal king of Goyim;
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
That these made war with Bera king of Sodom, and with Birsha king of Gomorrah, Shinab king of Admah, and Shemeber king of Zeboyim, and the king of Bela, which is Zoar.
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
All these joined together in the vale of Siddim, which is now the salt sea.
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Twelve years had they served Kedorlaomer, but in the thirteenth year they rebelled.
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
And in the fourteenth year came Kedorlaomer, and the kings that were with him, and they smote the Rephaim in Ashteroth-karnayim, and the Zuzim in Ham, and the Emim in Shaveh-kiriathayim,
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
And the Horites in their mountain Seir, unto El-paran, which is by the wilderness.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
And they returned and came to Enmishpat, which is Kadesh, and smote all the country of the Amalekites, and also the Emorites, that dwelt in Hazezon-tamar.
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
And then went out the king of Sodom, and the king of Gomorrah, and the king of Admah, and the king of Zeboyim, and the king of Bela, [the same is Zoar; ] and they joined battle with them in the vale of Siddim;
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
With Kedorlaomer king of Elam, and with Tidal king of Goyim, and Amraphel king of Shinar, and Arioch king of Ellasar; four kings with five.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
And the vale of Siddim was full of slime-pits; and the kings of Sodom and Gomorrah fled, and fell therein; and they that remained fled to the mountain.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
And they took all the goods of Sodom and Gomorrah, and all their victuals, and went their way.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
And they took Lot, Abram's brother's son, who dwelt in Sodom, and his goods, and departed.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
And there came one that had escaped, and told it to Abram the Hebrew; but he dwelt in the grove of Mamre the Emorite, brother of Eshcol, and brother of Aner, and these were confederates of Abram.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
And when Abram heard that his brother was taken captive, he armed his trained servants; born in his own house, three hundred and eighteen, and pursued them into Dan.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
And he divided himself against them, he and his servants, by night, and smote them, and pursued them unto Hobah, which is on the left hand of Damascus.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
And he brought back all the goods; and he also brought again his brother Lot, and his goods, and also the women, and the people.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
And the king of Sodom went out to meet him [after his return from smiting Kedorlaomer, and the kings that were with him] at the valley of Shaveh, which is the kings' dale.
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
And Malkizidek king of Salem brought forth bread and wine; and he was a priest of the most high God.
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
And he blessed him, and said, Blessed be Abram of the most high God, the possessor of heaven and earth.
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
And blessed he the most high God, who hath delivered thy enemies into thy hand. And he gave him tithes of all.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
And the king of Sodom said unto Abram, Give me the persons, and the goods take to thyself.
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
And Abram said to the king of Sodom, I have lifted up my hand unto the Lord, the most high God, the possessor of heaven and earth,
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
That I will not take from a thread even to a shoe-latchet, and that I will not take any thing that is thine; lest thou shouldst say, I have made Abram rich:
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
Save only that which the young men have eaten, and the portion of the men who went with me, Aner, Eshcol, and Mamre — these may take their portion.

< Mwanzo 14 >