< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
At that time Amraphel was king of Shinar, and he allied himself with Arioch, king of Ellasar, Chedorlaomer, king of Elam, and Tidal, king of Goiim.
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
They attacked Bera, king of Sodom, Birsha, king of Gomorrah, Shinab, king of Admah, Shemeber, king of Zeboiim, and the king of Bela (otherwise known as Zoar).
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
All these in the second group joined forces in the Valley of Siddim (the Dead Sea valley).
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
They had been under the rule of Chedorlaomer for twelve years, but in the thirteenth year they rebelled against him.
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
In the fourteenth year Chedorlaomer invaded, along with the kings in his alliance. They defeated the Rephaites in Ashteroth-karnaim, the Zuzites in Ham, the Emites in Shaveh-kiriathaim,
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
and the Horites in their hill country of Seir, all the way to El-paran, near the desert.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
Then they swung back through and attacked En-mishpat (otherwise known as Kadesh) and conquered the whole country belonging to the Amalekites, as well as the Amorites who lived in Hazazon-tamar.
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
Then the king of Sodom, the king of Gomorrah, the king of Admah, the king of Zeboiim, and the king of Bela (otherwise known as Zoar) marched out and prepared for battle in the Valley of Siddim.
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
They fought Chedorlaomer, king of Elam, Tidal, king of Goiim, Amraphel, king of Shinar, and Arioch, king of Ellasar—four kings on one side against five on the other.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
There were many tar pits in the Valley of Siddim, and as the defeated kings of Sodom and Gomorrah ran away, some of their men fell into them while the rest ran to the hills.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
The invaders took from Sodom and Gomorrah all their possessions and food and left.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
They also captured Lot, Abram's nephew, and his possessions, because he was living in Sodom.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
But one of those captured escaped and went and told Abram the Hebrew what had happened. Abram was living by the oaks of Mamre the Amorite, whose brothers were Eshcol and Aner. All of them were Abram's allies.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
When Abram found out that his nephew had been captured, he called together 318 fighting men who had been born in his household and chased after them all the way to Dan.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
There he divided his men into groups and attacked at night, defeating the enemy and chasing them as far as Hobah, north of Damascus.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
Abram recovered all that had been taken, including Lot and his possessions, and also brought back the women and others who had been captured.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
When Abram returned after defeating Chedorlaomer and his allies, the king of Sodom came out to meet him at the Valley of Shaveh (or Valley of the King).
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
Melchizedek, king of Salem, brought out bread and wine. He was a priest of the Most High God.
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
He blessed Abram, telling him, “May Abram be blessed by the Most High God, Creator of heaven and earth.
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
May the Most High God be praised, who handed your enemies over to you.” Then Abram gave Melchizedek one tenth of everything.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
The king of Sodom told Abram, “Let me have the people back, and you can keep everything else for yourself.”
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
But Abram replied to the king of Sodom, “I raise my hand, making a solemn promise to the Lord, the Most High God, Creator of heaven and earth,
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
that I refuse to take anything belonging to you, not a single thread or a sandal strap. Otherwise you might claim, ‘It was me who made Abram rich!’
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
I won't take anything except what my men have eaten, and the share for those who accompanied me—Aner, Eshcol, and Mamre. Let them have their share.”

< Mwanzo 14 >