< Mwanzo 14 >
1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
В дните не Сенаарския цар Амарфал, Еласарският цар Ариох, Еламският цар Ходологомор и Гоимският цар Тидал,
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
тия царе отвориха война против Содомския цар Вера, Гоморския цар Верса, Адманския цар Сенав, Цевоимския цар Симовор и царя на Вала, (която е Сигор).
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
Всички тия се събраха в Сидимската долина (дето е сега Соленото Море).
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Дванадесет години бяха се подчинявали на Ходологомора, а в тринадесетата въстанаха.
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
В четиринадесетата година дойдоха Ходологомор и царете, които бяха с него, та поразиха рафаимите в Астарот-карнаим, зузимите в Хам, емимите в Сави-кириатаим
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
и хорейците в поляната им Сиир, до Елфаран, който е при пустинята.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
А като се върнаха, дойдоха в Ен-мишнат, (който е Кадис), и поразиха цялата страна на амаликитяните, както и амореите, които живееха в Асасон-тамар.
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
Тогава Содомският цар, Гоморският цар, Адманският цар, Цевоимският цар и царят на Вала, (която е Сигор), излязоха и се опълчиха против тях на бой в Сидимската долина:
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
против Еламския цар Ходологомор, Гиомския цар Тидал, Сенаарския цар Амарфал и Еласарския цар Ариох. Имаше четирима царе против петимата.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
А Сидимската долина беше пълна със смолни кладенци; и Содомският и Гоморският царе, като бягаха, паднаха в тях, а останалите избягаха на бърдото.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
И победителите задигнаха всичкия имот на Содома и Гомора и всичката им храна и си отидоха.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
Взеха и Аврамовия братанец Лот, който живееше в Содом, заедно с имота му и си отидоха.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
А един от избавилите се дойде и извести това на евреина Аврам; той живееше при дъбовете на Амореца Мамврий, брат на Есхола и брат на Анера, които бяха Аврамови съюзници.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
А като чу Аврам, че брат му бил пленен, изведе своите триста и осемнадесет обучени мъже, родени в неговия дом и гони неприятеля до Дан.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
И през нощта, той и слугите му, като се разделиха против тях, поразиха ги и ги гониха до Хова, която е от ляво на Дамаск.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
И възвърна всичкия имот, върна на брата си Лота с имота му, както и жените и людете.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
И като се върна Аврам от поражението на Ходологомора и на царете, които бяха с него, Содомският цар излезе да го посрещне в Савинската долина, (която е Царевата долина).
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
Така Салимският цар Мелхиседек, който беше свещеник на Всемогъщия Бог, изнесе хляб и вино
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
та го благослови, казвайки: Благословен да бъде Аврам от Всевишния Бог, Създател на небето и на земята;
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
благословен и Всевишният Бог, който предаде неприятелите ти в твоята ръка. И Аврам му даде десетък от всичко.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
А Содомският цар рече на Аврама: Дай ми човеците, а имота задръж за себе си.
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
Но Аврам каза на Содомския цар: Аз дигнах ръката си пред Господа, Всевишния Бог, Създател на небето и земята,
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
и се заклех, че няма да взема нищо от твоето, ни конец ни ремък за обуща, да не би да речеш: Аз обогатих Аврама.
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
Приемам само онова, което изядоха момците; и дела на мъжете които отидоха с мене: Анер, Есхол и Мамври - те нека вземат дела си.