< Mwanzo 13 >

1 Hivyo Abramu akakwea kutoka Misri kwenda Negebu, yeye na mkewe na kila kitu alichokuwa nacho, pia Loti akaenda pamoja naye.
and to ascend: rise Abram from Egypt he/she/it and woman: wife his and all which to/for him and Lot with him [the] Negeb [to]
2 Wakati huo Abramu alikuwa tajiri sana wa mifugo, fedha na dhahabu.
and Abram heavy much in/on/with livestock in/on/with silver: money and in/on/with gold
3 Kutoka Negebu, akapita mahali hadi mahali, hadi akafika Betheli, mahali hapo ambapo mwanzoni alipiga hema lake kati ya Betheli na Ai
and to go: went to/for journey his from Negeb and till Bethel Bethel till [the] place which to be there (tent his *Q(K)*) in/on/with beginning between Bethel Bethel and between [the] Ai
4 hapo ambapo alikuwa amejenga madhabahu ya kwanza. Huko Abramu akaliitia jina la Bwana.
to(wards) place [the] altar which to make there in/on/with first and to call: call to there Abram in/on/with name LORD
5 Basi Loti, ambaye alikuwa anafuatana na Abramu, alikuwa pia na makundi ya mbuzi, kondoo, ngʼombe na mahema.
and also to/for Lot [the] to go: went with Abram to be flock and cattle and tent
6 Lakini nchi haikuwatosha kukaa pamoja kwa ajili ya wingi wa mali zao.
and not to lift: aid [obj] them [the] land: country/planet to/for to dwell together for to be property their many and not be able to/for to dwell together
7 Ukazuka ugomvi kati ya wachunga mifugo wa Abramu na wale wa Loti. Wakati huo, Wakanaani na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo.
and to be strife between to pasture livestock Abram and between to pasture livestock Lot and [the] Canaanite and [the] Perizzite then to dwell in/on/with land: country/planet
8 Hivyo Abramu akamwambia Loti, “Pasiwe na ugomvi wowote kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wako, kwa kuwa sisi ni ndugu.
and to say Abram to(wards) Lot not please to be provocation between me and between you and between to pasture my and between to pasture your for human brother: male-relative we
9 Je, nchi yote haiko mbele yako? Tutengane. Kama ukielekea kushoto, nitakwenda kulia; kama ukielekea kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
not all [the] land: country/planet to/for face: before your to separate please from upon me if [the] left and to go right and if [the] right and to go left
10 Loti akatazama akaona lile bonde lote la Yordani kuwa lilikuwa na maji tele, kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri, kuelekea Soari. (Hii ilikuwa kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora.)
and to lift: look Lot [obj] eye his and to see: see [obj] all talent [the] Jordan for all her irrigation to/for face: before to ruin LORD [obj] Sodom and [obj] Gomorrah like/as garden LORD like/as land: country/planet Egypt to come (in): towards you Zoar
11 Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana:
and to choose to/for him Lot [obj] all talent [the] Jordan and to set out Lot from front: east and to separate man: anyone from upon brother: male-sibling his
12 Abramu akaishi katika nchi ya Kanaani, wakati Loti aliishi miongoni mwa miji ya lile bonde na kupiga mahema yake karibu na Sodoma.
Abram to dwell in/on/with land: country/planet Canaan and Lot to dwell in/on/with city [the] talent and to pitch till Sodom
13 Basi watu wa Sodoma walikuwa waovu, wakifanya sana dhambi dhidi ya Bwana.
and human Sodom bad: evil and sinner to/for LORD much
14 Baada ya Loti kuondoka Bwana akamwambia Abramu, “Ukiwa hapo ulipo, inua macho yako utazame kaskazini na kusini, mashariki na magharibi.
and LORD to say to(wards) Abram after to separate Lot from from with him to lift: look please eye your and to see: see from [the] place which you(m. s.) there north [to] and south [to] and east [to] and sea: west [to]
15 Nchi yote unayoiona nitakupa wewe na uzao wako hata milele.
for [obj] all [the] land: country/planet which you(m. s.) to see: see to/for you to give: give her and to/for seed: children your till forever: enduring
16 Nitaufanya uzao wako uwe mwingi kama mavumbi ya nchi, hivyo kama kuna yeyote awezaye kuhesabu mavumbi, basi uzao wako utahesabika.
and to set: make [obj] seed: children your like/as dust [the] land: soil which if be able man: anyone to/for to count [obj] dust [the] land: soil also seed: children your to count
17 Ondoka, tembea katika marefu na mapana ya nchi, kwa maana ninakupa wewe.”
to arise: rise to go: walk in/on/with land: country/planet to/for length her and to/for width her for to/for you to give: give her
18 Basi Abramu akaondoa mahema yake, akaenda kuishi karibu na mialoni ya Mamre huko Hebroni, huko akamjengea Bwana madhabahu.
and to pitch Abram and to come (in): come and to dwell in/on/with terebinth Mamre which in/on/with Hebron and to build there altar to/for LORD

< Mwanzo 13 >