< Mwanzo 13 >

1 Hivyo Abramu akakwea kutoka Misri kwenda Negebu, yeye na mkewe na kila kitu alichokuwa nacho, pia Loti akaenda pamoja naye.
Therefore, Abram ascended from Egypt, he and his wife, and all that he had, and Lot with him, toward the southern region.
2 Wakati huo Abramu alikuwa tajiri sana wa mifugo, fedha na dhahabu.
But he was very wealthy by the possession of gold and silver.
3 Kutoka Negebu, akapita mahali hadi mahali, hadi akafika Betheli, mahali hapo ambapo mwanzoni alipiga hema lake kati ya Betheli na Ai
And he returned by the way that he came, from the meridian into Bethel, all the way to the place where before he had pitched his tent, between Bethel and Hai.
4 hapo ambapo alikuwa amejenga madhabahu ya kwanza. Huko Abramu akaliitia jina la Bwana.
There, at the place of the altar he had made before, he again called upon the name of the Lord.
5 Basi Loti, ambaye alikuwa anafuatana na Abramu, alikuwa pia na makundi ya mbuzi, kondoo, ngʼombe na mahema.
But Lot also, who was with Abram, had flocks of sheep, and cattle, and tents.
6 Lakini nchi haikuwatosha kukaa pamoja kwa ajili ya wingi wa mali zao.
Neither was the land able to contain them, so that they might dwell together. Indeed, their substance was so great that they could not live in common.
7 Ukazuka ugomvi kati ya wachunga mifugo wa Abramu na wale wa Loti. Wakati huo, Wakanaani na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo.
And then there also arose a conflict between the shepherds of Abram and of Lot. Now at that time the Canaanite and the Perizzite lived in that land.
8 Hivyo Abramu akamwambia Loti, “Pasiwe na ugomvi wowote kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wako, kwa kuwa sisi ni ndugu.
Therefore, Abram said to Lot: “I ask you, let there be no quarrel between me and you, and between my shepherds and your shepherds. For we are brothers.
9 Je, nchi yote haiko mbele yako? Tutengane. Kama ukielekea kushoto, nitakwenda kulia; kama ukielekea kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
Behold, the entire land is before your eyes. Withdraw from me, I beg you. If you will go to the left, I will take the right. If you choose the right, I will pass to the left.”
10 Loti akatazama akaona lile bonde lote la Yordani kuwa lilikuwa na maji tele, kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri, kuelekea Soari. (Hii ilikuwa kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora.)
And so Lot, lifting up his eyes, saw all the region around the Jordan, which was thoroughly irrigated, before the Lord overthrew Sodom and Gomorrah. It was like the Paradise of the Lord, and it was like Egypt, approaching toward Zoar.
11 Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana:
And Lot chose for himself the region around the Jordan, and he withdrew by way of the east. And they were divided, one brother from the other.
12 Abramu akaishi katika nchi ya Kanaani, wakati Loti aliishi miongoni mwa miji ya lile bonde na kupiga mahema yake karibu na Sodoma.
Abram dwelt in the land of Canaan. In truth, Lot stayed in the towns that were around the Jordan, and he lived in Sodom.
13 Basi watu wa Sodoma walikuwa waovu, wakifanya sana dhambi dhidi ya Bwana.
But the men of Sodom were very wicked, and they were sinners before the Lord beyond measure.
14 Baada ya Loti kuondoka Bwana akamwambia Abramu, “Ukiwa hapo ulipo, inua macho yako utazame kaskazini na kusini, mashariki na magharibi.
And the Lord said to Abram, after Lot was divided from him: “Lift up your eyes, and gaze out from the place where you are now, to the north and to the meridian, to the east and to the west.
15 Nchi yote unayoiona nitakupa wewe na uzao wako hata milele.
All the land that you see, I will give to you, and to your offspring even forever.
16 Nitaufanya uzao wako uwe mwingi kama mavumbi ya nchi, hivyo kama kuna yeyote awezaye kuhesabu mavumbi, basi uzao wako utahesabika.
And I will make your offspring like the dust of the earth. If any man is able to number the dust of the earth, he will be able to number your offspring as well.
17 Ondoka, tembea katika marefu na mapana ya nchi, kwa maana ninakupa wewe.”
Arise and walk through the land in its length, and breadth. For I will give it to you.”
18 Basi Abramu akaondoa mahema yake, akaenda kuishi karibu na mialoni ya Mamre huko Hebroni, huko akamjengea Bwana madhabahu.
Therefore, moving his tent, Abram went and dwelt by the steep valley of Mamre, which is in Hebron. And he built an altar there to the Lord.

< Mwanzo 13 >