< Mwanzo 12 >
1 Bwana akawa amemwambia Abramu, “Ondoka kutoka nchi yako, uache jamii yako na nyumba ya baba yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.
And Jehovah saith unto Abram, 'Go for thyself, from thy land, and from thy kindred, and from the house of thy father, unto the land which I shew thee.
2 “Mimi nitakufanya taifa kubwa na nitakubariki, Nitalikuza jina lako, nawe utakuwa baraka.
And I make thee become a great nation, and bless thee, and make thy name great; and be thou a blessing.
3 Nitawabariki wale wanaokubariki, na yeyote akulaaniye nitamlaani; na kupitia kwako mataifa yote duniani yatabarikiwa.”
And I bless those blessing thee, and him who is disesteeming thee I curse, and blessed in thee have been all families of the ground.'
4 Hivyo Abramu akaondoka kama Bwana alivyokuwa amemwambia; naye Loti akaondoka pamoja naye. Wakati Abramu alipoitwa aondoke Harani, alikuwa na miaka sabini na mitano.
And Abram goeth on, as Jehovah hath spoken unto him, and Lot goeth with him, and Abram [is] a son of five and seventy years in his going out from Charan.
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe pamoja na Loti mwana wa ndugu yake, mali zote walizokuwa nazo pamoja na watu aliokuwa amewapata huko Harani, wakasafiri mpaka nchi ya Kanaani, wakafika huko.
And Abram taketh Sarai his wife, and Lot his brother's son, and all their substance that they have gained, and the persons that they have obtained in Charan; and they go out to go towards the land of Canaan; and they come in to the land of Canaan.
6 Abramu akasafiri katika nchi hiyo akafika huko Shekemu, mahali penye mti wa mwaloni ulioko More. Wakati huo Wakanaani walikuwa wanaishi katika nchi hiyo.
And Abram passeth over into the land, unto the place Shechem, unto the oak of Moreh; and the Canaanite [is] then in the land.
7 Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Hivyo hapa akamjengea madhabahu Bwana aliyekuwa amemtokea.
And Jehovah appeareth unto Abram, and saith, 'To thy seed I give this land;' and he buildeth there an altar to Jehovah, who hath appeared unto him.
8 Kutoka huko Abramu akasafiri kuelekea kwenye vilima mashariki ya Betheli, naye akapiga hema huko, Betheli ikiwa upande wa magharibi na Ai upande wa mashariki. Huko alimjengea Bwana madhabahu na akaliitia jina la Bwana.
And he removeth from thence towards a mountain at the east of Beth-El, and stretcheth out the tent (Beth-El at the west, and Hai at the east), and he buildeth there an altar to Jehovah, and preacheth in the name of Jehovah.
9 Kisha Abramu akasafiri kuelekea upande wa Negebu.
And Abram journeyeth, going on and journeying towards the south.
10 Basi kulikuwako na njaa katika nchi, naye Abramu akashuka kwenda Misri kukaa huko kwa muda, kwa maana njaa ilikuwa kali.
And there is a famine in the land, and Abram goeth down towards Egypt to sojourn there, for the famine [is] grievous in the land;
11 Alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “Ninajua ya kwamba wewe ni mwanamke mzuri wa sura.
and it cometh to pass as he hath drawn near to enter Egypt, that he saith unto Sarai his wife, 'Lo, I pray thee, I have known that thou [art] a woman of beautiful appearance;
12 Wakati Wamisri watakapokuona, watasema, ‘Huyu ni mke wake.’ Ndipo wataniua, lakini wewe watakuacha hai.
and it hath come to pass that the Egyptians see thee, and they have said, 'This [is] his wife,' and they have slain me, and thee they keep alive:
13 Sema wewe ni dada yangu, ili nitendewe mema kwa ajili yako, na maisha yangu yatahifadhiwa kwa sababu yako.”
say, I pray thee, thou [art] my sister, so that it is well with me because of thee, and my soul hath lived for thy sake.'
14 Abramu alipoingia Misri, Wamisri wakamwona Sarai kuwa ni mwanamke mzuri sana wa sura.
And it cometh to pass, at the entering of Abram into Egypt, that the Egyptians see the woman that she [is] exceeding fair;
15 Maafisa wa Farao walipomwona, wakamsifia kwa Farao; ndipo Sarai akapelekwa kwa nyumba ya mfalme.
and princes of Pharaoh see her, and praise her unto Pharaoh, and the woman is taken [to] Pharaoh's house;
16 Kwa ajili ya Sarai, Farao akamtendea Abramu mema, naye Abramu akapata kondoo, ngʼombe, punda, ngamia na watumishi wa kiume na wa kike.
and to Abram he hath done good because of her, and he hath sheep and oxen, and he-asses, and men-servants, and handmaids, and she-asses, and camels.
17 Lakini Bwana akamwadhibu Farao na nyumba yake kwa maradhi ya kufisha kwa sababu ya kumchukua Sarai, mke wa Abramu.
And Jehovah plagueth Pharaoh and his house — great plagues — for the matter of Sarai, Abram's wife.
18 Ndipo Farao akamwita Abramu, akamuuliza, “Umenifanyia nini? Kwa nini hukuniambia ni mke wako?
And Pharaoh calleth for Abram, and saith, 'What [is] this thou hast done to me? why hast thou not declared to me that she [is] thy wife?
19 Kwa nini ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’ hata nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa basi, mke wako huyu hapa. Mchukue uende zako!”
Why hast thou said, She [is] my sister, and I take her to myself for a wife? and now, lo, thy wife, take and go.'
20 Kisha Farao akawapa watu wake amri kuhusu Abramu, wakamsindikiza pamoja na mke wake na kila alichokuwa nacho.
And Pharaoh chargeth men concerning him, and they send him away, and his wife, an all that he hath.