< Mwanzo 12 >
1 Bwana akawa amemwambia Abramu, “Ondoka kutoka nchi yako, uache jamii yako na nyumba ya baba yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.
Тогава Господ каза на Аврама: Излез от отечеството си, измежду рода си и из бащиния си дом, та иди в земята, която ще ти покажа.
2 “Mimi nitakufanya taifa kubwa na nitakubariki, Nitalikuza jina lako, nawe utakuwa baraka.
Ще те направя голям народ; ще те благословя, и ще прославя името ти, и ще бъдеш за благословение.
3 Nitawabariki wale wanaokubariki, na yeyote akulaaniye nitamlaani; na kupitia kwako mataifa yote duniani yatabarikiwa.”
Ще благословя ония, които те благославят, а ще прокълна всеки, който те кълне; и в тебе ще се благославят всички земни племена.
4 Hivyo Abramu akaondoka kama Bwana alivyokuwa amemwambia; naye Loti akaondoka pamoja naye. Wakati Abramu alipoitwa aondoke Harani, alikuwa na miaka sabini na mitano.
И тъй, Аврам тръгна според както му рече Господ, и Лот тръгна с него. А Аврам беше на седемдесет и пет години, когато излезе от Харан.
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe pamoja na Loti mwana wa ndugu yake, mali zote walizokuwa nazo pamoja na watu aliokuwa amewapata huko Harani, wakasafiri mpaka nchi ya Kanaani, wakafika huko.
Аврам взе жена си Сарайя, братанеца си Лот, всичкия имот, който бяха спечелили, и хората, които бяха придобили в Харан, та излязоха, за да отидат в Ханаанската земя.
6 Abramu akasafiri katika nchi hiyo akafika huko Shekemu, mahali penye mti wa mwaloni ulioko More. Wakati huo Wakanaani walikuwa wanaishi katika nchi hiyo.
И Аврам пропътува земята до местността Сихем, до дъба Море. В това време ханаанците живееха в земята.
7 Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Hivyo hapa akamjengea madhabahu Bwana aliyekuwa amemtokea.
И Господ се яви на Аврама и рече: На твоето потомство ще дам тая земя. И там издигна олтар на Господа, Който му се яви.
8 Kutoka huko Abramu akasafiri kuelekea kwenye vilima mashariki ya Betheli, naye akapiga hema huko, Betheli ikiwa upande wa magharibi na Ai upande wa mashariki. Huko alimjengea Bwana madhabahu na akaliitia jina la Bwana.
От там се премести към хълма, който е на изток от Ветил, дето разпъна шатрата си, Ветил оставаше на запад, а Гай - на изток; и там издигна олтар на Господа и призова Господното име.
9 Kisha Abramu akasafiri kuelekea upande wa Negebu.
После, като се дигна, Аврам все напредваше към юг.
10 Basi kulikuwako na njaa katika nchi, naye Abramu akashuka kwenda Misri kukaa huko kwa muda, kwa maana njaa ilikuwa kali.
А настана глад в земята; затова Аврам слезе в Египет да поживее там, понеже гладът беше се усилил в Ханаанската земя.
11 Alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “Ninajua ya kwamba wewe ni mwanamke mzuri wa sura.
И когато наближи да влезе в Египет, рече на жена си Сарайя: Виж сега, зная, че си жена красива наглед.
12 Wakati Wamisri watakapokuona, watasema, ‘Huyu ni mke wake.’ Ndipo wataniua, lakini wewe watakuacha hai.
Египтяните, като те видят, ще рекат: Тя му е жена; и мене ще убият, а тебе ще оставят жива.
13 Sema wewe ni dada yangu, ili nitendewe mema kwa ajili yako, na maisha yangu yatahifadhiwa kwa sababu yako.”
Кажи, моля, че си ми сестра, за да ми бъда добре покрай тебе и да се опази живота ми, поради твоята дума.
14 Abramu alipoingia Misri, Wamisri wakamwona Sarai kuwa ni mwanamke mzuri sana wa sura.
И като влезе Аврам в Египет, египтяните видяха, че жената беше твърде красива.
15 Maafisa wa Farao walipomwona, wakamsifia kwa Farao; ndipo Sarai akapelekwa kwa nyumba ya mfalme.
Видяха я и Фараоновите големци и я похвалиха на Фараона; затова жената беше заведена в дома на Фараона.
16 Kwa ajili ya Sarai, Farao akamtendea Abramu mema, naye Abramu akapata kondoo, ngʼombe, punda, ngamia na watumishi wa kiume na wa kike.
И заради нея той стори добро на Аврама, който достигна да има овци, говеда, осли, слуги, слугини, ослици и камили.
17 Lakini Bwana akamwadhibu Farao na nyumba yake kwa maradhi ya kufisha kwa sababu ya kumchukua Sarai, mke wa Abramu.
Но Господ порази Фараона и дома му с тежки язви, поради Аврамовата жена Сарайя.
18 Ndipo Farao akamwita Abramu, akamuuliza, “Umenifanyia nini? Kwa nini hukuniambia ni mke wako?
Тогава Фараон повика Аврама и рече: Що е това, което ти ми стори? Защо не ми каза, че ти е жена?
19 Kwa nini ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’ hata nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa basi, mke wako huyu hapa. Mchukue uende zako!”
Защо ми каза: Сестра ми е, така че аз си я взех за жена; сега, прочее, ето жена ти; вземи я и си иди.
20 Kisha Farao akawapa watu wake amri kuhusu Abramu, wakamsindikiza pamoja na mke wake na kila alichokuwa nacho.
И Фараон му определи човеци, които изпратиха него, жена му и всичко що имаше.