< Mwanzo 11 >
1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
Entonces toda la tierra tenía una sola lengua y las mismas palabras.
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
Aconteció que al salir hacia el oriente, encontraron una llanura en la tierra de Sinar y se establecieron allí.
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
Entonces se dijeron unos a otros: Vengan, fabriquemos adobes y quemémoslos con fuego. El ladrillo les sirvió en lugar de piedra, y el asfalto en lugar de argamasa.
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
Y dijeron: Vengan, construyámonos una ciudad y una torre cuya cúspide llegue al cielo. Hagámonos un nombre, en caso de que seamos esparcidos por la superficie de toda la tierra.
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
Pero Yavé descendió para ver la ciudad y la torre que edificaban los hijos de los hombres.
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
Y Yavé dijo: Ciertamente son un pueblo y todos ellos tienen la misma lengua. Éste es solo el principio de su obra y nada les hará desistir de lo que planean hacer.
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
Vamos, descendamos ya y confundamos allí su lengua para que nadie entienda el lenguaje del otro.
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
Yavé los dispersó de allí por toda la superficie de la tierra, y desistieron de construir la ciudad.
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
Por eso lo llamó Babel, porque allí Yavé confundió la lengua de toda la tierra. Desde allí Yavé los esparció por la superficie de toda la tierra.
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
Estos son los descendientes de Sem: Cuando Sem tenía 100 años engendró a Arfaxad, dos años después del diluvio.
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Sem vivió después de engendrar a Arfaxad 500 años, y engendró hijos e hijas.
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
Arfaxad vivió 35 años y engendró a Sala.
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Arfaxad vivió 403 años después que engendró a Sala, y engendró hijos e hijas.
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Sala vivió 30 años y engendró a Heber.
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Sala vivió después de engendrar a Heber 403 años, y engendró hijos e hijas.
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Heber vivió 34 años y engendró a Peleg.
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Heber vivió después de engendrar a Peleg 430 años, y engendró hijos e hijas.
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
Peleg vivió 30 años y engendró a Reú.
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Peleg vivió 209 años después de engendrar a Reú, y engendró hijos e hijas.
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
Reú vivió 32 años y engendró a Serug.
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Reú vivió después de engendrar a Serug 207 años, y engendró hijos e hijas.
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Serug vivió 30 años y engendró a Nacor.
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Después de engendrar a Nacor, Serug vivió 200 años, y engendró hijos e hijas.
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Nacor vivió 29 años y engendró a Taré.
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Nacor vivió después de engendrar a Taré 119 años, y engendró hijos e hijas.
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
Y Taré vivió 70 años y engendró a Abram, a Nacor y a Harán.
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
Estos son los descendientes de Taré: Taré engendró a Abram, a Nacor y a Harán. Harán engendró a Lot.
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
Pero Harán murió antes que su padre Taré en la tierra de su nacimiento, Ur de los caldeos.
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
Abram y Nacor tomaron para ellos esposas. El nombre de la esposa de Abram era Saray y el de la esposa de Nacor era Milca, hija de Harán, padre de Milca y de Isca.
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
Saray era estéril. No tenía hijos.
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
Taré tomó a Abram, su hijo, a Lot, su nieto, hijo de Harán, y a Saray, su nuera, esposa de su hijo Abram, y salieron de Ur de los caldeos para ir a la tierra de Canaán. Pero llegaron hasta Harán y se establecieron allí.
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
Los días de Taré fueron 205 años, y murió en Harán.