< Mwanzo 11 >
1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
Erat autem terra labii unius, et sermonum eorumdem.
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
Cumque proficiscerentur de oriente, invenerunt campum in terra Sennaar, et habitaverunt in eo.
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
Dixitque alter ad proximum suum: Venite, faciamus lateres, et coquamus eos igni. Habueruntque lateres pro saxis, et bitumen pro caemento:
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
et dixerunt: Venite, faciamus nobis civitatem et turrim, cuius culmen pertingat ad caelum: et celebremus nomen nostrum antequam dividamur in universas terras.
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
Descendit autem Dominus ut videret civitatem et turrim, quam aedificabant filii Adam,
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
et dixit: Ecce, unus est populus, et unum est labium omnibus: coeperuntque hoc facere, nec desistent a cogitationibus suis, donec eas opere compleant.
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
Venite igitur, descendamus, et confundamus ibi linguam eorum, ut non audiat unusquisque vocem proximi sui.
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
Atque ita divisit eos Dominus ex illo loco in universas terras, et cessaverunt aedificare civitatem.
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
Et idcirco vocatum est nomen eius Babel, quia ibi confusum est labium universae terrae: et inde dispersit eos Dominus super faciem cunctarum regionum.
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
Hae sunt generationes Sem: Sem erat centum annorum quando genuit Arphaxad, biennio post diluvium.
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sem postquam genuit Arphaxad, quingentis annis: et genuit filios et filias.
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
Porro Arphaxad vixit triginta quinque annis, et genuit Sale.
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Arphaxad postquam genuit Sale, trecentis tribus annis: et genuit filios et filias.
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Sale quoque vixit triginta annis, et genuit Heber.
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sale postquam genuit Heber, quadringentis tribus annis: et genuit filios et filias.
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Vixit autem Heber triginta quattuor annis, et genuit Phaleg.
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Heber postquam genuit Phaleg, quadringentis triginta annis: et genuit filios et filias.
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
Vixit quoque Phaleg triginta annis, et genuit Reu.
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Phaleg postquam genuit Reu, ducentis novem annis, et genuit filios et filias.
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
Vixit autem Reu triginta duobus annis, et genuit Sarug.
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixit quoque Reu postquam genuit Sarug, ducentis septem annis: et genuit filios et filias.
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Vixit vero Sarug triginta annis, et genuit Nachor.
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sarug postquam genuit Nachor, ducentis annis: et genuit filios et filias.
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Vixit autem Nachor viginti novem annis, et genuit Thare.
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Nachor postquam genuit Thare, centum decem et novem annis: et genuit filios et filias.
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
Vixitque Thare septuaginta annis, et genuit Abram et Nachor, et Aran.
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
Hae sunt autem generationes Thare: Thare genuit Abram, Nachor, et Aran. Porro Aran genuit Lot.
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
Mortuusque est Aran ante Thare patrem suum, in terra nativitatis suae in Ur Chaldaeorum.
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
Duxerunt autem Abram et Nachor uxores: nomen uxoris Abram, Sarai: et nomen uxoris Nachor, Melcha filia Aran patris Melchae, et patris Ieschae.
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
Erat autem Sarai sterilis, nec habebat liberos.
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
Tulit itaque Thare Abram filium suum, et Lot filium Aran, filium filii sui, et Sarai nurum suam, uxorem Abram filii sui, et eduxit eos de Ur Chaldaeorum, ut irent in terram Chanaan: veneruntque usque Haran, et habitaverunt ibi.
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
Et facti sunt dies Thare ducentorum quinque annorum, et mortuus est in Haran.