< Mwanzo 11 >

1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
全地は一の言語一の音のみなりき
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
茲に人衆東に移りてシナルの地に平野を得て其處に居住り
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
彼等互に言けるは去來甎石を作り之を善く爇んと遂に石の代に甎石を獲灰沙の代に石漆を獲たり
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
又曰けるは去來邑と塔とを建て其塔の頂を天にいたらしめん斯して我等名を揚て全地の表面に散ることを免れんと
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
ヱホバ降臨りて彼人衆の建る邑と塔とを觀たまへり
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
ヱホバ言たまひけるは視よ民は一にして皆一の言語を用ふ今既に此を爲し始めたり然ば凡て其爲んと圖維る事は禁止め得られざるべし
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
去來我等降り彼處にて彼等の言語を淆し互に言語を通ずることを得ざらしめんと
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
ヱホバ遂に彼等を彼處より全地の表面に散したまひければ彼等邑を建ることを罷たり
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
是故に其名はバベル(淆亂)と呼ばる是はヱホバ彼處に全地の言語を淆したまひしに由てなり彼處よりヱホバ彼等を全地の表に散したまへり
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
セムの傳は是なりセム百歳にして洪水の後の二年にアルパクサデを生り
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
セム、アルパクサデを生し後五百年生存へて男子女子を生り
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
アルパクサデ三十五歳に及びてシラを生り
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
アルパクサデ、シラを生し後四百三年生存へて男子女子を生り
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
シラ三十歳におよびてエベルを生り
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
シラ、エベルを生し後四百三年生存へて男子女子を生り
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
エベル三十四歳におよびてペレグを生り
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
エベル、ペレグを生し後四百三十年生存へて男子女子を生り
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
ペレグ三十歳におよびてリウを生り
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ペレグ、リウを生し後二百九年生存へて男子女子を生り
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
リウ三十二歳におよびてセルグを生り
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
リウ、セルグを生し後二百七年生存へて男子女子を生り
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
セルグ三十年におよびてナホルを生り
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
セルグ、ナホルを生しのち二百年生存へて男子女子を生り
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
ナホル二十九歳に及びてテラを生り
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ナホル、テラを生し後百十九年生存へて男子女子を生り
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
テラ七十歳に及びてアブラム、ナホルおよびハランを生り
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
テラの傳は是なりテラ、アブラム、ナホルおよびハランを生ハラン、ロトを生り
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
ハランは其父テラに先ちて其生處なるカルデアのウルにて死たり
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
アブラムとナホルと妻を娶れりアブラムの妻の名をサライと云ナホルの妻の名をミルカと云てハランの女なりハランはミルカの父にして亦イスカの父なりき
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
サライは石女にして子なかりき
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
テラ、カナンの地に往とて其子アブラムとハランの子なる其孫ロト及其子アブラムの妻なる其媳サライをひき挈て倶にカルデアのウルを出たりしがハランに至て其處に住り
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
テラの齡は二百五歳なりきテラはハランにて死り

< Mwanzo 11 >