< Mwanzo 11 >

1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
And the whole earth is of one language, and of the same words,
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
and it comes to pass, in their journeying from the east, that they find a valley in the land of Shinar and dwell there;
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
and they each say to his neighbor, “Give help, let us make bricks, and burn [them] thoroughly”: and the brick is to them for stone, and the bitumen has been to them for mortar.
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
And they say, “Give help, let us build for ourselves a city and tower with its head in the heavens, and make for ourselves a name, lest we be scattered over the face of all the earth.”
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
And YHWH comes down to see the city and the tower which the sons of men have built;
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
and YHWH says, “Behold, the people [is] one, and one language [is] to them all, and this it has dreamed of doing; and now, nothing is restrained from them of that which they have purposed to do.
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
Give help, let us go down there and confuse their language, so that a man will not understand the language of his companion.”
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
And YHWH scatters them from there over the face of all the earth, and they cease to build the city;
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
therefore [one] has called its name Babel, for there YHWH has confused the language of all the earth, and from there YHWH has scattered them over the face of all the earth.
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
These [are] the generations of Shem: Shem [is] a son of one hundred years, and begets Arphaxad two years after the flood.
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Shem lives after his begetting Arphaxad five hundred years, and begets sons and daughters.
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
And Arphaxad has lived thirty-five years [[or one hundred and thirty-five years]], and begets Salah.
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Arphaxad lives after his begetting Salah four hundred and three years [[or four hundred and thirty years]], and begets sons and daughters.
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
And Salah has lived thirty years [[or one hundred and thirty years]], and begets Eber.
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Salah lives after his begetting Eber four hundred and three years [[or three hundred and thirty years]], and begets sons and daughters.
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
And Eber lives thirty-four years [[or one hundred and thirty-four years]], and begets Peleg.
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Eber lives after his begetting Peleg four hundred and thirty years [[or three hundred and seventy years]], and begets sons and daughters.
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
And Peleg lives thirty years [[or one hundred and thirty years]], and begets Reu.
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Peleg lives after his begetting Reu two hundred and nine years, and begets sons and daughters.
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
And Reu lives thirty-two years [[or one hundred and thirty-two years]], and begets Serug.
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Reu lives after his begetting Serug two hundred and seven years, and begets sons and daughters.
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
And Serug lives thirty years [[or one hundred and thirty years]], and begets Nahor.
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Serug lives after his begetting Nahor two hundred years, and begets sons and daughters.
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
And Nahor lives twenty-nine years [[or seventy-nine years]], and begets Terah.
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Nahor lives after his begetting Terah one hundred and nineteen years [[or one hundred and twenty-nine years]], and begets sons and daughters.
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
And Terah lives seventy years, and begets Abram, Nahor, and Haran.
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
And these [are] the generations of Terah: Terah has begotten Abram, Nahor, and Haran; and Haran has begotten Lot;
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
and Haran dies in the presence of Terah his father, in the land of his birth, in Ur of the Chaldees.
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
And Abram and Nahor take to themselves wives; the name of Abram’s wife [is] Sarai, and the name of Nahor’s wife [is] Milcah, daughter of Haran, father of Milcah, and father of Iscah.
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
And Sarai is barren—she has no child.
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
And Terah takes his son Abram, and Lot, son of Haran, his son’s son, and his daughter-in-law Sarai, wife of his son Abram, and they go out with them from Ur of the Chaldees, to go toward the land of Canaan; and they come to Haran, and dwell there.
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
And the days of Terah are two hundred and five years, and Terah dies in Haran.

< Mwanzo 11 >