< Mwanzo 11 >
1 Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
And the whole earth was of one language and of one speech.
2 Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
And it came to pass, as they journeyed east, that they found a plain in the land of Shinar, and they dwelt there.
3 Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
And they said one to another, Come, let us make brick, and burn them thoroughly. And they had brick for stone, and they had slime for mortar.
4 Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
And they said, Come, let us build a city for us, and a tower, and its top in the heavens. And let us make a name for us, lest we be scattered abroad upon the face of the whole earth.
5 Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
And Jehovah came down to see the city and the tower, which the sons of men built.
6 Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
And Jehovah said, Behold, they are one people, and they have all one language, and this is what they begin to do. And now nothing will be withheld from them, which they propose to do.
7 Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
Come, let us go down, and there confound their language, that they may not understand each other's speech.
8 Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
So Jehovah scattered them abroad from there upon the face of all the earth, and they left off building the city.
9 Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
Therefore the name of it was called Babel, because Jehovah there confounded the language of all the earth, and from there Jehovah scattered them abroad upon the face of all the earth.
10 Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
These are the generations of Shem. Shem was a hundred years old, and begot Arphaxad two years after the flood.
11 Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Shem lived five hundred years after he begot Arphaxad, and begot sons and daughters.
12 Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
And Arphaxad lived a hundred and thirty-five years, and begot Cainan.
13 Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Arphaxad lived after he had begotten Cainan, four hundred years, and begot sons and daughters, and died. And Cainan lived a hundred and thirty years and begot Shelah; and Cainan lived after he had begotten Shelah, three hundred and thirty years, and begot sons and daughters, and died.
14 Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
And Shelah lived thirty years, and begot Eber.
15 Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Shelah lived four hundred and three years after he begot Eber, and begot sons and daughters.
16 Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
And Eber lived thirty-four years, and begot Peleg.
17 Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Eber lived four hundred and thirty years after he begot Peleg, and begot sons and daughters.
18 Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
And Peleg lived thirty years, and begot Reu.
19 Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Peleg lived two hundred and nine years after he begot Reu, and begot sons and daughters.
20 Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
And Reu lived thirty-two years, and begot Serug.
21 Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Reu lived two hundred and seven years after he begot Serug, and begot sons and daughters.
22 Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
And Serug lived thirty years, and begot Nahor.
23 Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Serug lived two hundred years after he begot Nahor, and begot sons and daughters.
24 Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
And Nahor lived twenty-nine years, and begot Terah.
25 Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Nahor lived a hundred and nineteen years after he begot Terah, and begot sons and daughters.
26 Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
And Terah lived seventy years, and begot Abram, Nahor, and Haran.
27 Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
Now these are the generations of Terah: Terah begot Abram, Nahor, and Haran. And Haran begot Lot.
28 Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
And Haran died before his father Terah in the land of his nativity, in Ur of the Chaldees.
29 Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
And Abram and Nahor took wives to themselves. The name of Abram's wife was Sarai, and the name of Nahor's wife, Milcah, the daughter of Haran, the father of Milcah, and the father of Iscah.
30 Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
And Sarai was barren; she had no child.
31 Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
And Terah took Abram his son, and Lot the son of Haran, his son's son, and Sarai his daughter-in-law, his son Abram's wife. And they went forth with them from Ur of the Chaldees, to go into the land of Canaan. And they came to Haran, and dwelt there.
32 Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.
And the days of Terah were two hundred and five years, and Terah died in Haran.