< Mwanzo 10 >
1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Estos son los descendientes de Sem, Cam y Jafet, hijos de Noé, a quienes les nacieron hijos después del diluvio.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
Los hijos de Jafet: Gomer, Magog, Madai, Javán, Tubal, Mesec y Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
Los hijos de Gomer: Askenaz, Rifat y Togarma.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Los hijos de Javán: Elisha, Tarsis, Kitim y Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
A partir de estos fueron pobladas las costas, cada uno en sus territorios, según su lengua, por sus familias en sus naciones.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Los hijos de Cam: Cus, Mizraim, Fut y Canaán.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Los hijos de Cus: Seba, Havila, Sabta, Raama y Sabteca. Los hijos de Raama: Seba y Dedán.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Cus también engendró a Nimrod, el cual comenzó a ser poderoso en la tierra.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
Él fue intrépido cazador enfrentado a Yavé. Por esto se dice: Como Nimrod, intrépido cazador enfrentado a Yavé.
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
El principio de su reino fue Babel, Erec, Acad y Calne, en tierra de Sinar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
Salió de aquella tierra, y al ser fortalecido, edificó Nínive, Ciudad Rehobot, Cala
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
y Resen, entre Nínive y Cala, la cual es una ciudad grande.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
Mizraim engendró a Ludim, a Anamim, a Lehabim, a Naftuhim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
a Patrusim, a Casluhim, de donde salieron los filisteos, y a Caftorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Canaán engendró a Sidón, su primogénito, a Het,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
al jebuseo, al amorreo al gergeseo,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
al heveo, al araceo, al sineo,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
al arvadeo, al zemareo y al hemateo. Después se dispersaron las familias de los cananeos.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
La frontera del cananeo iba desde Sidón en dirección a Gerar, hasta Gaza, y en dirección de Sodoma, Gomorra, Adma y Zeboim, hasta Lasa.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Estos son los hijos de Cam por sus familias y sus lenguas, sus territorios y sus naciones.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
También le nacieron hijos a Sem, padre de todos los hijos de Heber, y hermano mayor de Jafet.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Los hijos de Sem fueron Elam, Asur, Arfaxad, Lud y Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
Los hijos de Aram fueron Uz, Hul, Geter y Mas.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
Arfaxad engendró a Sala, y Sala engendró a Heber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
A Heber le nacieron dos hijos: El nombre del primero fue Peleg, porque en sus días la tierra fue dividida. El nombre de su hermano fue Joctán.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Joctán engendró a Almodad, a Selef, a Hazar-mavet, a Jera,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
a Adoram, a Uzal, a Dicla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
a Obal, a Abimael, a Seba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
a Ofir, a Havila y a Jobab. Todos éstos fueron hijos de Joctán.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Su vivienda fue desde Mesa en dirección a Sefar, en la montaña oriental.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Estos son los hijos de Sem según sus familias, sus lenguas y sus tierras en sus naciones.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
Tales fueron los hijos de Noé por sus familias en sus naciones. De éstas fueron divididas las naciones de la tierra después del diluvio.