< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Hae sunt generationes filiorum Noe, Sem, Cham, et Iapheth: natique sunt eis filii post diluvium.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
Filii Iapheth: Gomer, et Magog, et Madai, et Iavan, et Thubal, et Mosoch, et Thiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
Porro filii Gomer: Ascenez et Riphath et Thogorma.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Filii autem Iavan: Elisa et Tharsis, Cetthim et Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
Ab his divisae sunt insulae gentium in regionibus suis, unusquisque secundum linguam suam et familias suas in nationibus suis.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Filii autem Cham: Chus, et Mesraim, et Phuth, et Chanaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Filii autem Chus: Saba, et Hevila, et Sabatha, et Regma, et Sabatacha. Filii Regma: Saba, et Dadan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Porro Chus genuit Nemrod: ipse coepit esse potens in terra,
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
et erat robustus venator coram Domino. Ob hoc exivit proverbium: Quasi Nemrod robustus venator coram Domino.
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
Fuit autem principium regni eius Babylon, et Arach, et Achad, et Chalanne, in terra Sennaar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
De terra illa egressus est Assur, et aedificavit Niniven, et plateas civitatis, et Chale.
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
Resen quoque inter Niniven et Chale: haec est civitas magna.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
At vero Mesraim genuit Ludim, et Anamim, et Laabim, et Nephthuim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
et Phetrusim, et Chasluim: de quibus egressi sunt Philisthiim et Caphtorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Chanaan autem genuit Sidonem primogenitum suum, Hethaeum,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
et Iebusaeum, et Amorrhaeum, et Gergesaeum,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
et Hevaeum, et Aracaeum: Sinaeum,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
et Aradium, Samaraeum et Amathaeum: et per hos disseminati sunt populi Chananaeorum.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
Factique sunt termini Chanaan venientibus a Sidone Geraram usque ad Gazam, donec ingrediaris Sodomam et Gomorrham, et Adamam, et Seboim usque Lasa.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Hi sunt filii Cham in cognationibus, et linguis, et generationibus, terrisque et gentibus suis.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
De Sem quoque nati sunt, patre omnium filiorum Heber, fratre Iapheth maiore.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Filii Sem: Aelam et Assur, et Arphaxad, et Lud, et Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
Filii Aram: Us, et Hul, et Gether, et Mes.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
At vero Arphaxad genuit Sale, de quo ortus est Heber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
Natique sunt Heber filii duo: nomen uni Phaleg, eo quod in diebus eius divisa sit terra: et nomen fratris eius Iectan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Qui Iectan genuit Elmodad, et Saleph, et Asarmoth, Iare,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
et Aduram, et Uzal, et Decla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
et Ebal, et Abimael, Saba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
et Ophir, et Hevila, et Iobab. omnes isti, filii Iectan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Et facta est habitatio eorum de Messa pergentibus usque Sephar montem orientalem.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Isti sunt filii Sem secundum cognationes et linguas, et regiones in gentibus suis.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
Hae familiae Noe iuxta populos et nationes suas. Ab his divisae sunt gentes in terra post diluvium.

< Mwanzo 10 >