< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
ノアの子セム、ハム、ヤペテの系図は次のとおりである。洪水の後、彼らに子が生れた。
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
ヤペテの子孫はゴメル、マゴグ、マダイ、ヤワン、トバル、メセク、テラスであった。
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
ゴメルの子孫はアシケナズ、リパテ、トガルマ。
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
ヤワンの子孫はエリシャ、タルシシ、キッテム、ドダニムであった。
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
これらから海沿いの地の国民が分れて、おのおのその土地におり、その言語にしたがい、その氏族にしたがって、その国々に住んだ。
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
ハムの子孫はクシ、ミツライム、プテ、カナンであった。
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
クシの子孫はセバ、ハビラ、サブタ、ラアマ、サブテカであり、ラアマの子孫はシバとデダンであった。
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
クシの子はニムロデであって、このニムロデは世の権力者となった最初の人である。
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
彼は主の前に力ある狩猟者であった。これから「主の前に力ある狩猟者ニムロデのごとし」ということわざが起った。
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
彼の国は最初シナルの地にあるバベル、エレク、アカデ、カルネであった。
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
彼はその地からアッスリヤに出て、ニネベ、レホボテイリ、カラ、
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
およびニネベとカラとの間にある大いなる町レセンを建てた。
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
ミツライムからルデ族、アナミ族、レハビ族、ナフト族、
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
パテロス族、カスル族、カフトリ族が出た。カフトリ族からペリシテ族が出た。
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
カナンからその長子シドンが出て、またヘテが出た。
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
その他エブスびと、アモリびと、ギルガシびと、
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
ヒビびと、アルキびと、セニびと、
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
アルワデびと、ゼマリびと、ハマテびとが出た。後になってカナンびとの氏族がひろがった。
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
カナンびとの境はシドンからゲラルを経てガザに至り、ソドム、ゴモラ、アデマ、ゼボイムを経て、レシャに及んだ。
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
これらはハムの子孫であって、その氏族とその言語とにしたがって、その土地と、その国々にいた。
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
セムにも子が生れた。セムはエベルのすべての子孫の先祖であって、ヤペテの兄であった。
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
セムの子孫はエラム、アシュル、アルパクサデ、ルデ、アラムであった。
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
アラムの子孫はウヅ、ホル、ゲテル、マシであった。
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
アルパクサデの子はシラ、シラの子はエベルである。
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
エベルにふたりの子が生れた。そのひとりの名をペレグといった。これは彼の代に地の民が分れたからである。その弟の名をヨクタンといった。
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
ヨクタンにアルモダデ、シャレフ、ハザルマウテ、エラ、
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
ハドラム、ウザル、デクラ、
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
オバル、アビマエル、シバ、
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
オフル、ハビラ、ヨバブが生れた。これらは皆ヨクタンの子であった。
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
彼らが住んだ所はメシャから東の山地セパルに及んだ。
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
これらはセムの子孫であって、その氏族とその言語とにしたがって、その土地と、その国々にいた。
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
これらはノアの子らの氏族であって、血統にしたがって国々に住んでいたが、洪水の後、これらから地上の諸国民が分れたのである。

< Mwanzo 10 >