< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Or ce sont ici les générations des enfants de Noé, Sem, Cam et Japheth; auxquels naquirent des enfants après le déluge.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
Les enfants de Japheth sont Gomer, Magog, Madaï, Javan, Tubal, Mésech, et Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
Et les enfants de Gomer, Askénaz, Riphath, et Thogarma.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Et les enfants de Javan, Elisa, Tarsis, Kittim, et Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
De ceux-là furent divisées les Iles des nations par leurs terres, chacun selon sa langue, selon leurs familles, entre leurs nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Et les enfants de Cam sont Cus, Mitsraïm, Put, et Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Et les enfants de Cus: Séba, Havila, Sabtah, Rahma, et Sebtéca. Et les enfants de Rahma, Séba, et Dédan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Cus engendra aussi Nimrod, qui commença d'être puissant sur la terre.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
Il fut un puissant chasseur devant l'Eternel; c'est pourquoi l'on a dit: Comme Nimrod, le puissant chasseur devant l'Eternel.
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
Et le commencement de son règne fut Babel, Erec, Accad, et Calné au pays de Sinhar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
De ce pays-là sortit Assur, et il bâtit Ninive, et les rues de la ville, et Calah,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
Et Résen, entre Ninive et Calah, qui est une grande ville.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
Mitsraïm engendra Ludim, Hanamim, Léhabim, Naphtuhim.
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
Pathrusim, Chasluhim, desquels sont issus les Philistins, et Caphtorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Et Canaan engendra Sidon, son fils aîné, et Heth,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
Les Jébusiens, les Amorrhéens, les Guirgasiens,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
Les Héviens, les Harkiens, et les Siniens,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
Les Arvadiens, les Tsémariens, et les Hamathiens. Et ensuite les familles des Cananéens se sont dispersées.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
Et les limites des Cananéens furent depuis Sidon, quand on vient vers Guérar, jusqu'à Gaza, en tirant vers Sodome et Gomorrhe, Adma, et Tséboïm, jusqu'à Lésa.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Ce sont là les enfants de Cam selon leurs familles [et leurs] langues, en leurs pays, et en [leurs] nations.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
Et il naquit des enfants à Sem, père de tous les enfants d'Héber, et frère de Japheth, [qui était] le plus grand.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Et les enfants de Sem sont Hélam, Assur, Arpacsad, Lud, et Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
Et les enfants d'Aram, Hus, Hul, Guéther et Mas.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
Et Arpacsad engendra Sélah, et Sélah engendra Héber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
Et à Héber naquirent deux fils: le nom de l'un fut Péleg, parce qu'en son temps la terre fut partagée; et le nom de son frère fut Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Et Joktan engendra Almodad, Séleph, Hatsarmaveth, et Jérah.
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
Hadoram, Uzal, Dikla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Hobal, Abimaël, Séba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ophir, Havila, et Jobab. Tous ceux-là sont les enfants de Joktan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Et leur demeure était depuis Mésa, quand on vient en Séphar, montagne d'Orient.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Ce sont là les enfants de Sem, selon leurs familles [et] leurs langues, en leurs pays, et en [leurs] nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
Telles sont les familles des enfants de Noé, selon leurs lignées en leurs nations; et de ceux-là ont été divisées les nations sur la terre après le déluge.

< Mwanzo 10 >