< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Voici la postérité des fils de Noé, Sem, Cham et Japheth. Il leur naquit des fils après le déluge.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
Fils de Japheth: Gomer, Magog, Madaï, Javan, Thubal, Mosoch et Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
Fils de Gomer: Ascénez, Riphath et Thogorma. —
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Fils de Javan: Elisa et Tharsis, Cetthim et Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
C'est d'eux que viennent les peuples dispersés dans les îles des nations, dans leurs divers pays, chacun selon sa langue, selon leurs familles, selon leurs nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Fils de Cham: Chus, Mesraïm, Phuth et Chanaan. —
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Fils de Chus: Saba, Hévila, Sabatha, Regma et Sabathaca. Fils de Regma: Saba et Dadan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Chus engendra Nemrod: celui-ci fut le premier un homme puissant sur la terre.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
Ce fut un vaillant chasseur devant Yahweh; c'est pourquoi l'on dit: " Comme Nemrod, vaillant chasseur devant Yahweh. "
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
Le commencement de son empire fut Babel, Arach, Achad et Chalanné au pays de Sennaar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
De ce pays il alla en Assur, et bâtit Ninive, Rechoboth-Ir, Chalé,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
et Résen, entre Ninive et Chalé; c'est la grande ville. —
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
Mesraïm engendra les Ludim, les Anamim, les Laabim, les Nephthuim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
les Phétrusim, les Chasluim, d'où sont sortis les Philistins, et les Caphtorim. —
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Chanaan engendra Sidon, son premier-né, et Heth,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
ainsi que les Jébuséens, les Amorrhéens, les Gergéséens,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
les Hévéens, les Aracéens, les Sinéens,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
les Aradiens, les Samaréens et les Hamathéens. Ensuite les familles des Chananéens se répandirent dans le pays,
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
et le territoire des Chananéens alla depuis Sidon, dans la direction de Gérare, jusqu'à Gaza; et, dans la direction de Sodome, Gomorrhe, Adama, et Séboïm, jusqu'à Lésa. —
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Tels sont les fils de Cham selon leurs familles, selon leurs langues, dans leurs divers pays, dans leurs nations.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
Des fils naquirent aussi à Sem, qui est le père de tous les fils d'Héber et le frère aîné de Japheth.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Fils de Sem: Elam, Assur, Arphaxad, Lud et Aram. —
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
Fils d'Aram: Us, Hul, Géther et Mes. —
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
Arphaxad engendra Salé, et Salé engendra Héber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
Et il naquit à Héber deux fils: le nom de l'un était Phaleg, parce que de son temps la terre était partagée, et le nom de son frère était Jectan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Jectan engendra Elmodad, Saleph, Asarmoth, Jaré,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
Aduram, Uzal, Décla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Ebal, Abimaël, Saba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ophir, Hévila et Jobab. Tous ceux-là sont fils de Jectan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Le pays qu'ils habitèrent fut la montagne d'Orient, à partir de Mésa, dans la direction de Séphar. —
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
Tels sont les fils de Sem, selon leurs familles, selon leurs langues, dans leurs divers pays, selon leurs nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
Telles sont les familles des fils de Noé selon leurs générations, dans leurs nations. C'est d'eux que sont sorties les nations qui se sont répandues sur la terre après le déluge.

< Mwanzo 10 >