< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
The following are the genealogies of the sons of Noah: Shem, Ham, and Japheth. They had sons born to them after the flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
The sons of Japheth: Gomer, Magog, Madai, Javan, Tubal, Meshech, and Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
The sons of Gomer: Ashkenaz, Riphath, and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
The sons of Javan: Elishah, Tarshish, Kittim, and Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
The descendants of these ancestors spread throughout the coastal areas, each group having their own language, with their families developing into different nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
The sons of Ham: Cush, Mizraim, Put, and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
The sons of Cush: Seba, Havilah, Sabtah, Raamah, and Sabteca. The sons of Raamah: Sheba and Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Cush was also the father of Nimrod, who set himself up as the first tyrant on earth.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
He was a powerful fighter who defied the Lord; which is why there's the expression, “Like Nimrod, a powerful fighter who defied the Lord.”
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
His kingdom began in the cities of Babel, Erech, Akkad, and Calneh, all located in the land of Shinar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
From there he moved into Assyria and built the cities of Nineveh, Rehoboth-Ir, Calah,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
and Resen, which lies between Nineveh and the great city of Calah.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
Mizraim was the father of the Ludites, the Anamites, the Lehabites, the Naphtuhites,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
the Pathrusites, the Casluhites, and the Caphtorites (ancestors of the Philistines).
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Canaan was the father of Sidon, his firstborn, and of the Hittites,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
the Jebusites, the Amorites, the Girgashites,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
the Hivites, the Arkites, the Sinites,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
the Arvadites, the Zemarites, and the Hamathites. Later the Canaanite tribes spread out
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
and the territory of the Canaanites stretched from Sidon towards Gerar and all the way to Gaza, then towards Sodom, Gomorrah, Admah, and Zeboiim, all the way to Lasha.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These were the sons of Ham according to their tribes, languages, lands, and nation.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
Shem, whose older brother was Japheth, also had sons. Shem was the forefather of all the sons of Eber.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
The sons of Shem: Elam, Asshur, Arphaxad, Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
The sons of Aram: Uz, Hul, Gether, and Mash.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
Arphaxad was the father of Shelah. Shelah was the father of Eber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
Eber had two sons. One was named Peleg, because in his time the earth was divided; the name of his brother was Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Joktan was the father of Almodad, Sheleph, Hazarmaveth, Jerah,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
Hadoram, Uzal, Diklah,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Obal, Abimael, Sheba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ophir, Havilah, and Jobab. These were all sons of Joktan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
They lived in the land lying between Mesha to Sephar, in the hill country to the east.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These were the sons of Shem, according to their tribes, languages, lands, and nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
These were all the tribes descended from Noah's sons, according to their genealogies and national groups. From these ancestors the different nations of the earth spread around the world after the flood.

< Mwanzo 10 >