< Mwanzo 10 >
1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
These are the generations of the sons of Noah: Shem, Ham, and Japheth, and of the sons who were born to them after the great flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
The sons of Japheth were Gomer, and Magog, and Madai, and Javan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
And then the sons of Gomer were Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
And the sons of Javan were Elishah, and Tarshish, Kittim, and Rodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
The islands of the Gentiles were divided by these into their regions, each one according to his tongue, and their families in their nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
And the Sons of Ham were Cush, and Mizraim, and Put, and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
And the sons of Cush were Seba, and Havilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabteca. The sons of Raamah were Sheba and Dadan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
And then Cush conceived Nimrod; he began to be powerful on the earth.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
And he was an able hunter before the Lord. From this, a proverb came forth: ‘Just like Nimrod, an able hunter before the Lord.’
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
And so, the beginning of his kingdom was Babylon, and Erech, and Accad, and Chalanne, in the land of Shinar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
From that land, Assur came forth, and he built Nineveh, and the streets of the city, and Calah,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
and also Resen, between Nineveh and Calah. This is a great city.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
And truly, Mizraim conceived Ludim, and Anamim, and Lehabim, Naphtuhim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
and Pathrusim, and Casluhim, from whom came forth the Philistines and the Caphtorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Then Canaan conceived Sidon his firstborn, the Hittite,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
and the Jebusite, and the Amorite, the Girgashite,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
the Hivite, and the Arkite: the Sinite,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
and the Arvadian, the Samarite, and the Hamathite. And after this, the peoples of the Canaanites became widespread.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
And the borders of Canaan went, as one travels, from Sidon to Gerar, even to Gaza, until one enters Sodom and Gomorrah, and from Admah and Zeboiim, even to Lesa.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Ham in their kindred, and tongues, and generations, and lands, and nations.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
Likewise, from Shem, the father of all the sons of Heber, the elder brother of Japheth, sons were born.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
The sons of Shem were Elam, and Asshur, and Arphaxad, and Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
The sons of Aram were Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
But truly, Arphaxad conceived Shelah, from whom was born Eber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
And to Eber were born two sons: the name of the one was Peleg, for in his days the earth became divided, and his brother’s name was Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
This Joktan conceived Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, Jerah
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
and Hadoram, and Uzal and Diklah,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
and Obal and Abimael, Sheba
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
and Ophir, and Havilah and Jobab. All these were the sons of Joktan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
And their habitation extended from Messa, as one sojourns, even to Sephar, a mountain in the east.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Shem according to their kindred, and tongues, and the regions within their nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
These are the families of Noah, according to their peoples and nations. The nations became divided according to these, on the earth after the great flood.