< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Now these are the generations of the sons of Noah, of Shem, Ham, and Japheth. And sons were born to them after the flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
The sons of Japheth: Gomer, and Magog, and Madai, and Javan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
And the sons of Gomer: Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
And the sons of Javan: Elishah, and Tarshish, Kittim, and Dodanim.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
From these were the islands of the nations divided in their lands, every man according to his tongue, according to their families, in their nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
And the sons of Ham: Cush, and Mizraim, and Put, and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
And the sons of Cush: Seba, and Havilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabteca. And the sons of Raamah: Sheba, and Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
And Cush begot Nimrod. He began to be a mighty man on the earth.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
He was a mighty hunter before Jehovah. Therefore it is said, Like Nimrod a mighty hunter before Jehovah.
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
And the beginning of his kingdom was Babel, and Erech, and Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
He went forth out of that land into Assyria, and built Nineveh, and Rehoboth-ir, and Calah,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
and Resen between Nineveh and Calah (the same is the great city).
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
And Mizraim begot Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
and Pathrusim, and Casluhim (from where the Philistines went forth), and Caphtorim.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
And Canaan begot Sidon his firstborn, and Heth,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
and the Jebusite, and the Amorite, and the Girgashite,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
and the Hivite, and the Arkite, and the Sinite,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
and the Arvadite, and the Zemarite, and the Hamathite. And afterward the families of the Canaanite were spread abroad.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
And the border of the Canaanite was from Sidon, as thou go toward Gerar, to Gaza, as thou go toward Sodom and Gomorrah and Admah and Zeboiim, to Lasha.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Ham, according to their families, according to their tongues, in their lands, in their nations.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
And to Shem, the father of all the sons of Eber, the elder brother of Japheth, sons were also born to him.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
The sons of Shem: Elam, and Asshur, and Arphaxad, and Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
And the sons of Aram: Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
And Arphaxad begot Shelah, and Shelah begot Eber.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
And to Eber were born two sons. The name of the one was Peleg. For in his days the earth was divided. And his brother's name was Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
And Joktan begot Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
and Hadoram, and Uzal, and Diklah,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
and Obal, and Abimael, and Sheba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
and Ophir, and Havilah, and Jobab. All these were the sons of Joktan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
And their dwelling was from Mesha, as thou go toward Sephar, the mountain of the east.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These are the sons of Shem, according to their families, according to their tongues, in their lands, according to their nations.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
These are the families of the sons of Noah, according to their generations, in their nations. And from these the nations were divided on the earth after the flood.

< Mwanzo 10 >