< Mwanzo 10 >
1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
Ovo je povijest Noinih sinova: Šema, Hama i Jafeta, kojima su se rodili sinovi poslije Potopa.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
Sinovi su Jafetovi: Gomer, Magog, Madaj, Javan, Tubal, Mešak, Tiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
A sinovi su Gomerovi: Aškenaz, Rifat i Togarma.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Javanovi su opet sinovi: Eliša, Taršiš, Kitijci i Dodanci.
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
Od njih su se razgranali narodi po otocima. To su Jafetovi sinovi prema svojim zemljama - svaki s vlastitim jezikom - prema svojim plemenima i narodima.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Sinovi su Hamovi: Kuš i Misrajim, Put i Kanaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Kuševi su: Seba, Havila, Sabta, Rama i Sabteka. Ramini su: Šeba i Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Od Kuša se rodio Nimrod, koji je postao prvi velmoža na zemlji.
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
Voljom Jahve bio je silan lovac. Zato se veli: “Kao Nimrod, silan lovac voljom Jahve.”
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
Glavno uporište njegova kraljevstva bili su: Babilon, Erek, Akad i Kalne, svi u zemlji Šinearu.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
Iz ove je zemlje došao Ašur. On je podigao Ninivu, Rehobot Ir, Kalah
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
i Resen između Ninive i Kalaha (to je glavni grad).
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
Od Misrajima potekli su Ludijci, Anamijci, Lehabijci, Naftuhijci,
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
pa Patrušani, Kasluhijci i Kaftorci, od kojih su potekli Filistejci.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Od Kanaana potječe Sidon, njegov prvenac, i Het.
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
Dalje: Jebusejci, Amorejci, Girgašani,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
Hivijci, Arkijci, Sinijci,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
Arvađani, Semarjani i Hamaćani. Poslije se kanaanska plemena razgranaše,
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
tako da se granica Kanaanaca protezala od Sidona prema Geraru sve do Gaze pa prema Sodomi, Gomori, Admi i Sebojimu sve do Leše.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
To su sinovi Hamovi prema svojim plemenima i jezicima, po svojim zemljama i narodima.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
A i Šemu - praocu svih sinova Eberovih i starijem bratu Jafetovu - rodili se sinovi.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
Šemovi su sinovi: Elam, Ašur, Arpakšad, Lud i Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
A Aramovi su sinovi: Us, Hul, Geter i Maš.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
Arpakšad rodi Šelaha, Šelah rodi Ebera.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
Eberu su se rodila dva sina: jednomu bješe ime Peleg, jer se za njegova vijeka zemlja razdijelila. Njegovu je bratu bilo ime Joktan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Od Joktana se rodiše: Almodad, Šelef, Hasarmavet, Jerah,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
Hadoram, Uzal, Dikla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Obal, Abimael, Šeba,
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ofir, Havila i Jobab. Sve su to sinovi Joktanovi.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
Njihova se naselja protezahu od Meše sve do Sefara, brdovitih krajeva na istoku.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
To su sinovi Šemovi prema svojim plemenima, jezicima i zemljama, po svojim narodima.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
To su rodovi Noinih sinova prema svojim lozama i narodima. Od njih su se razgranali narodi po zemlji poslije Potopa.