+ Mwanzo 1 >

1 Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
Au commencement, Dieu créa les cieux et la terre.
2 Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
La terre était informe et vide. Les ténèbres étaient à la surface de l'abîme et l'Esprit de Dieu planait au-dessus de la surface des eaux.
3 Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.
Dieu dit: « Que la lumière soit! » et la lumière fut.
4 Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema, ndipo Mungu akatenganisha nuru na giza.
Dieu vit la lumière, et il vit qu'elle était bonne. Dieu sépara la lumière d'avec les ténèbres.
5 Mungu akaiita nuru “mchana,” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.
Dieu appela la lumière « jour », et il appela les ténèbres « nuit ». Il y eut un soir et il y eut un matin: ce fut le premier jour.
6 Mungu akasema, “Iwepo nafasi kati ya maji igawe maji na maji.”
Dieu dit: « Qu'il y ait une étendue au milieu des eaux, et qu'elle sépare les eaux d'avec les eaux. »
7 Kwa hiyo Mungu akafanya nafasi, akatenganisha maji yaliyo chini ya hiyo nafasi na maji yaliyo juu yake. Ikawa hivyo.
Dieu fit l'étendue, et il sépara les eaux qui étaient au-dessous de l'étendue des eaux qui étaient au-dessus de l'étendue; et il en fut ainsi.
8 Mungu akaiita hiyo nafasi “anga.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
Dieu appela l'étendue « ciel ». Il y eut un soir et il y eut un matin, un second jour.
9 Mungu akasema, “Maji yaliyopo chini ya anga na yakusanyike mahali pamoja, pawepo na nchi kavu.” Ikawa hivyo.
Dieu dit: « Que les eaux qui sont sous le ciel se rassemblent en un seul lieu, et que la terre sèche apparaisse »; et il en fut ainsi.
10 Mungu akaiita nchi kavu “ardhi,” nalo lile kusanyiko la maji akaliita “bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.
Dieu appela la terre sèche « terre », et il appela le rassemblement des eaux « mer ». Dieu vit que cela était bon.
11 Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe mimea: miche itoayo mbegu, miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo.
Dieu dit: « Que la terre produise de l'herbe, des herbes portant des graines, et des arbres fruitiers portant des fruits selon leur espèce, avec leurs graines, sur la terre ».
12 Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu kulingana na aina zake, na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake. Mungu akaona ya kuwa hili ni jema.
La terre produisit de l'herbe, des herbes portant de la semence selon leur espèce, et des arbres fruitiers portant du fruit selon leur espèce, avec leur semence en elle; et Dieu vit que cela était bon.
13 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tatu.
Il y eut un soir, et il y eut un matin: ce fut le troisième jour.
14 Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,
Dieu dit: « Qu'il y ait des luminaires dans l'étendue du ciel pour séparer le jour d'avec la nuit, et qu'ils servent de signes pour marquer les saisons, les jours et les années;
15 nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.
et qu'ils servent de luminaires dans l'étendue du ciel pour éclairer la terre ».
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.
Dieu fit les deux grands luminaires: le grand luminaire pour régir le jour, et le petit luminaire pour régir la nuit. Il fit aussi les étoiles.
17 Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,
Dieu les plaça dans l'étendue du ciel pour éclairer la terre,
18 itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
pour dominer le jour et la nuit, et pour séparer la lumière des ténèbres. Dieu vit que cela était bon.
19 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne.
Il y eut un soir et il y eut un matin: ce fut le quatrième jour.
20 Mungu akasema, “Kuwepo na viumbe hai tele kwenye maji, nao ndege waruke juu ya dunia katika nafasi ya anga.”
Dieu dit: « Que les eaux regorgent d'êtres vivants, et que les oiseaux volent au-dessus de la terre dans l'étendue du ciel. »
21 Kwa hiyo Mungu akaumba viumbe wakubwa wa baharini na kila kiumbe hai kiendacho majini kulingana na aina zake, na kila ndege mwenye mabawa kulingana na aina yake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
Dieu créa les grands animaux marins et tous les êtres vivants qui se meuvent, dont les eaux fourmillent, selon leur espèce, et tout oiseau ailé selon son espèce. Dieu vit que cela était bon.
22 Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni mwongezeke, mkayajaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika dunia.”
Dieu les bénit, en disant: « Soyez féconds, multipliez, remplissez les eaux des mers, et que les oiseaux se multiplient sur la terre. »
23 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tano.
Il y eut un soir, et il y eut un matin: ce fut le cinquième jour.
24 Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana na aina zake: wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori, kila mnyama kulingana na aina yake.” Ikawa hivyo.
Dieu dit: « Que la terre produise des êtres vivants selon leur espèce, du bétail, des reptiles et des animaux de la terre selon leur espèce »; et il en fut ainsi.
25 Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
Dieu fit les animaux de la terre selon leur espèce, le bétail selon son espèce, et tout ce qui rampe sur le sol selon son espèce. Dieu vit que cela était bon.
26 Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.”
Dieu dit: « Faisons l'homme à notre image, selon notre ressemblance. Qu'ils dominent sur les poissons de la mer, sur les oiseaux du ciel, sur le bétail, sur toute la terre et sur tous les reptiles qui rampent sur la terre. »
27 Kwa hiyo Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanaume na mwanamke aliwaumba.
Dieu a créé l'homme à son image. Il le créa à l'image de Dieu; il les créa mâle et femelle.
28 Mungu akawabariki na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.”
Dieu les bénit. Dieu leur dit: « Soyez féconds, multipliez, remplissez la terre et soumettez-la. Dominez les poissons de la mer, les oiseaux du ciel et tout être vivant qui se meut sur la terre. »
29 Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa dunia yote, na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa chakula chenu.
Dieu dit: « Voici, je vous ai donné toute herbe portant de la semence, qui est à la surface de toute la terre, et tout arbre portant du fruit et portant de la semence. Ce sera votre nourriture.
30 Nao wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani, na viumbe vyote viendavyo juu ya ardhi: yaani kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila mche wa kijani kuwa chakula.” Ikawa hivyo.
A tout animal de la terre, à tout oiseau du ciel, et à tout ce qui rampe sur la terre et qui a de la vie, j'ai donné toute herbe verte pour nourriture.
31 Mungu akaona vyote alivyoumba, na tazama, ilikuwa vizuri sana. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.
Dieu vit tout ce qu'il avait fait, et voici, cela était très bon. Il y eut un soir et il y eut un matin, un sixième jour.

+ Mwanzo 1 >