+ Mwanzo 1 >

1 Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
In the beginning God created the heavens and the earth.
2 Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
And the earth was without form and void, and darkness was upon the face of the deep, and the Spirit of God moved upon the face of the waters.
3 Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.
And God said, Let there be light, and there was light.
4 Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema, ndipo Mungu akatenganisha nuru na giza.
And God saw the light, that it was good. And God divided the light from the darkness.
5 Mungu akaiita nuru “mchana,” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.
And God called the light Day, and the darkness he called Night. And there was evening and there was morning, one day.
6 Mungu akasema, “Iwepo nafasi kati ya maji igawe maji na maji.”
And God said, Let there be a firmament in the midst of the waters, and let it divide the waters from the waters.
7 Kwa hiyo Mungu akafanya nafasi, akatenganisha maji yaliyo chini ya hiyo nafasi na maji yaliyo juu yake. Ikawa hivyo.
And God made the firmament, and divided the waters which were under the firmament from the waters which were above the firmament. And it was so.
8 Mungu akaiita hiyo nafasi “anga.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
And God called the firmament Heaven. And there was evening and there was morning, a second day.
9 Mungu akasema, “Maji yaliyopo chini ya anga na yakusanyike mahali pamoja, pawepo na nchi kavu.” Ikawa hivyo.
And God said, Let the waters under the heavens be gathered together to one place, and let the dry land appear. And it was so.
10 Mungu akaiita nchi kavu “ardhi,” nalo lile kusanyiko la maji akaliita “bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.
And God called the dry land Earth, and he called the gathering together of the waters Seas. And God saw that it was good.
11 Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe mimea: miche itoayo mbegu, miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo.
And God said, Let the earth put forth grass, herbs yielding seed, and fruit trees bearing fruit according to their kind (in which is the seed of them) upon the earth. And it was so.
12 Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu kulingana na aina zake, na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake. Mungu akaona ya kuwa hili ni jema.
And the earth brought forth grass, herbs yielding seed according to their kind, and trees bearing fruit in which is the seed of it, according to their kind. And God saw that it was good.
13 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tatu.
And there was evening and there was morning, a third day.
14 Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,
And God said, Let there be lights in the firmament of heaven to divide the day from the night, and let them be for signs, and for seasons, and for days and years.
15 nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.
And let them be for lights in the firmament of heaven to give light upon the earth. And it was so.
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.
And God made the two great lights, the greater light to rule the day, and the lesser light to rule the night, also the stars.
17 Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,
And God set them in the firmament of heaven to give light upon the earth,
18 itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
and to rule over the day and over the night, and to divide the light from the darkness. And God saw that it was good.
19 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne.
And there was evening and there was morning, a fourth day.
20 Mungu akasema, “Kuwepo na viumbe hai tele kwenye maji, nao ndege waruke juu ya dunia katika nafasi ya anga.”
And God said, Let the waters swarm with swarms of living creatures, and let birds fly above the earth in the open firmament of heaven.
21 Kwa hiyo Mungu akaumba viumbe wakubwa wa baharini na kila kiumbe hai kiendacho majini kulingana na aina zake, na kila ndege mwenye mabawa kulingana na aina yake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
And God created the great sea creatures, and every living creature that moves, which the waters brought forth abundantly, according to their kind, and every winged bird according to its kind. And God saw that it was good.
22 Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni mwongezeke, mkayajaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika dunia.”
And God blessed them, saying, Be fruitful, and multiply, and fill the waters in the seas, and let birds multiply on the earth.
23 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tano.
And there was evening and there was morning, a fifth day.
24 Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana na aina zake: wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori, kila mnyama kulingana na aina yake.” Ikawa hivyo.
And God said, Let the earth bring forth living creatures according to their kind, cattle, and creeping things, and beasts of the earth according to their kind. And it was so.
25 Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
And God made the beasts of the earth according to their kind, and the cattle according to their kind, and everything that creeps upon the ground according to its kind. And God saw that it was good.
26 Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.”
And God said, Let us make mankind in our image-after our likeness-and let them have dominion over the fish of the sea, and over the birds of the heavens, and over the cattle, and over all the earth, and over every creeping thing that creeps upon the earth.
27 Kwa hiyo Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanaume na mwanamke aliwaumba.
And God created mankind in his own image, in the image of God he created him, male and female he created them.
28 Mungu akawabariki na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.”
And God blessed them. And God said to them, Be fruitful, and multiply, and fill the earth, and have power over it, and have dominion over the fish of the sea, and over the birds of the heavens, and over every living thing that moves upon the earth.
29 Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa dunia yote, na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa chakula chenu.
And God said, Behold, I have given you every herb yielding seed, which is upon the face of all the earth, and every tree, in which is the fruit of a tree yielding seed. To you it shall be for food,
30 Nao wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani, na viumbe vyote viendavyo juu ya ardhi: yaani kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila mche wa kijani kuwa chakula.” Ikawa hivyo.
and to every beast of the earth, and to every bird of the heavens, and to everything that creeps upon the earth in which there is life, for food-every green herb. And it was so.
31 Mungu akaona vyote alivyoumba, na tazama, ilikuwa vizuri sana. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.
And God saw everything that he had made, and, behold, it was very good. And there was evening and there was morning, the sixth day.

+ Mwanzo 1 >