< Wagalatia 1 >
1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an Apostle, not from men, neither by man; but by Jesus Christ, and God the Father who raised him from the dead;
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren who are with me, to the congregations of Galatia:
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Favor to you, and peace from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn )
who gave himself for our sins, that he might deliver us from the present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn )
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
to whom be the glory for ever and ever. Amen. (aiōn )
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I wonder that you are so soon removed from him who called you into the favor of Christ, to another gospel;
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
which is not another: but there are some who trouble you, and wish to pervert the gospel of Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But if even we, or an angel from heaven, declare a gospel to you, different from what we have declared to you, let him be accursed.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we said before, so now I say again, if any one declare a gospel to you, different from what you have received, let him be accursed.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For do I now conciliate men, or God? or do I seek to please men? for if I yet pleased men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
Now I certify you, brethren, concerning the gospel which was declared by me, that it is not according to men.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
For I neither received it from man, nor was I taught it, except by the revelation of Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
You have certainly heard of my behavior formerly in Judaism; that I exceedingly persecuted the congregation of God, and laid it waste;
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and made progress in Judaism above many of the same age with myself, in my own nation, being more exceedingly jealous of the traditions of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when God, who separated me from my mother's womb, and called me by his favor, was pleased
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
to reveal his Son to me, that I might declare the good news concerning him to the Gentiles; immediately I did not consult flesh and blood:
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
neither did I go up to Jerusalem, to them who were Apostles before me; but I went away in Arabia, and again returned to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then, after three years, I went up to Jerusalem, to become acquainted with Peter, and abode with him fifteen days.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
But I saw no other of the Apostles, except James, the Lord's brother.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Now as to the things which I write to you, behold, God is my witness that I do not falsely affirm.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
After that, I went into the regions of Syria and Cilicia;
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
and I was personally unknown to the congregations of Judea which are in Christ.
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
They had only heard that--he who formerly persecuted us, now announces, as glad tidings, the faith which he formerly destroyed.
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
And they glorified God on my account.