< Wagalatia 3 >
1 Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
O nespametni Galačani, kdo vas je uročil, da ne bi ubogali resnice, pred čigar očmi je bil očitno postavljen Jezus Kristus, križan med vami?
2 Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
Samo to hočem izvedeti od vas: »Ali ste prejeli Duha z deli postave ali s poslušnostjo veri?«
3 Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
Ali ste tako nespametni? Ali ste, začenši z Duhom, sedaj popolni v mesu?
4 Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
Ali ste toliko stvari pretrpeli zaman? Če bi bile vendarle zaman.
5 Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
On torej, ki vam daje Duha in med vami dela čudeže, ali jih dela po delih postave ali po poslušnosti veri?
6 Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
Celó kakor je Abraham veroval Bogu in mu je bilo to šteto za pravičnost.
7 Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
Spoznajte torej, da so Abrahamovi otroci tisti, ki so iz vere.
8 Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
In ker je pismo slutilo, da bo Bog pogane opravičil po veri, je poprej oznanjalo evangelij Abrahamu, rekoč: ›V tebi bodo blagoslovljeni vsi narodi.‹
9 Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
Tako so torej tisti, ki so iz vere, blagoslovljeni z zvestim Abrahamom.
10 Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
Kajti kolikor jih je iz del postave, so pod prekletstvom, kajti pisano je: ›Preklet je vsak, kdor ne vztraja v vseh stvareh, ki so pisane v knjigi postave, da jih izvrši.‹
11 Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
Toda očitno je to, da v Božjih očeh noben človek ni opravičen s postavo, kajti: ›Pravični bo živel iz vere.‹
12 Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
Postava pa ni iz vere, temveč: ›Človek, ki jih izvršuje, bo živel po njih.‹
13 Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
Kristus nas je odkupil od prekletstva postave, ko je za nas postal prekletstvo, kajti pisano je: ›Preklet je vsak, kdor visi na drevesu.‹
14 Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
Da bi Abrahamov blagoslov lahko po Jezusu Kristusu prešel na pogane, da bi mi po veri lahko prejeli obljubo Duha.
15 Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
Bratje, govorim po človeških običajih: »Čeprav je to samo človeška zaveza, vendar če je potrjena, je noben človek ne razveljavlja ali dodaja k njej.«
16 Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
Torej obljube so bile izrečene Abrahamu in njegovemu semenu. Ni rekel: ›In semenom, ‹ kakor mnogim; temveč kakor enemu: ›In tvojemu semenu, ‹ ki je Kristus.
17 Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
In pravim to, da zaveze, ki je bila prej potrjena od Boga v Kristusu, postava, ki je bila štiristo trideset let kasneje, ne more razveljaviti, da bi obljubo storila brez učinka.
18 Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
Kajti če je dediščina po postavi, le-ta ni več po obljubi; toda Bog jo je Abrahamu dal po obljubi.
19 Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
Čemu potem služi postava? Dodana je bila zaradi prestopkov, dokler ne bi prišel potomec, ki mu je bila dana obljuba; in ta je bila odrejena po angelih v roko posrednika.
20 Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
Torej posrednik ni posrednik enega, toda Bog je eden.
21 Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
Ali je potem postava zoper Božje obljube? Bog ne daj, kajti če bi bila dana postava, ki bi lahko dala življenje, bi bila pravičnost resnično po postavi.
22 Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
Toda pismo je vse zaprlo pod greh, da bi bila lahko tem, ki verujejo, dana obljuba po veri Jezusa Kristusa.
23 Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
Toda preden je prišla vera, smo bili držani pod postavo, zaprti veri, ki naj bi se razodela kasneje.
24 Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
Zatorej je bila postava naša vzgojiteljica, da nas privede h Kristusu, da bi bili mi lahko opravičeni iz vere.
25 Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
Toda potem, ko je prišla vera, nismo več pod vzgojiteljico.
26 Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
Kajti vi vsi ste Božji otroci po veri v Kristusa Jezusa.
27 Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
Kajti tako veliko, kot vas je bilo krščenih v Kristusa, ste oblekli Kristusa.
28 Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
Ni niti Juda niti Grka, ni niti sužnja niti svobodnega, ni niti moškega niti ženske; kajti vsi vi ste eno v Kristusu Jezusu.
29 Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.
Če pa ste Kristusovi, potem ste Abrahamovo seme in dediči glede na obljubo.