< Wagalatia 3 >

1 Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
O foolish Galatians, who bewitched you? before whose eyes Jesus Christ was plainly set forth among you crucified.
2 Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
This only I desire to learn from you: Was it from the works of the Law that ye received the Spirit, or by the preaching of faith?
3 Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
Are ye so foolish? Having begun with the Spirit, do ye now end with the flesh?
4 Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
Have ye suffered so much in vain? if indeed it be really in vain.
5 Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
Doth he then who is supplying to you the Spirit, and working miracles among you, do it by the works of the Law, or by the preaching of faith?
6 Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
Even as Abraham “believed God, and it was accounted to him as righteousness.”
7 Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
Know then that they who have faith, these are the sons of Abraham.
8 Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
Moreover the Scripture, foreseeing that God was to accept the gentiles as righteous by faith, proclaimed beforehand the glad tidings to Abraham, saying, “In thee shall all nations be blessed.”
9 Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
So then they who have faith are blessed with believing Abraham.
10 Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
For as many as rely on the works of the Law are under a curse; for it is written, “Cursed is every one that continueth not in all things which are written in the book of the Law, to do them.”
11 Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
But further, that through the observance of the Law no one is accepted as righteous with God is evident; for “the righteous shall live by faith.”
12 Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
And the Law hath nothing to do with faith; but [[its language is]], “He that hath done them shall live in them.”
13 Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
Christ redeemed us from the curse of the Law, having become a curse for us; for it is written, “Cursed is every one that is hanged on a beam of wood,”—
14 Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
to the end that in Christ Jesus the blessing promised to Abraham might come to the gentiles, that we through faith might receive the Spirit which was promised.
15 Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
Brethren, I speak according to what is practised among men; no one sets aside even a human covenant, or makes additions to it, after it has been ratified.
16 Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
But the promises were made to Abraham and “to his offspring.” He doth not say, “and to offsprings,” as speaking of many, but, as speaking of one, “and to thy offspring,” which is Christ.
17 Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
And what I mean is this; that a covenant that was before ratified by God, the Law, which came four hundred and thirty years after, cannot annul, so as to make void the promise;
18 Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
for if the inheritance cometh from the Law, it ceaseth to be the consequence of the promise; but to Abraham God gave it by promise.
19 Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
To what end then was the Law? It was added because of transgressions, till the offspring should come to whom the promise belongeth, having been ordained through angels by the hand of a mediator.
20 Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
Now no mediator is a mediator of one; but God is one.
21 Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
Is then the Law against the promises of God? Far be it! For if a law had been given which was able to give life, righteousness would indeed have been by the Law;
22 Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
but the Scripture shut up all under sin, that the blessing promised through faith in Jesus Christ might be given to those who believe.
23 Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
But before faith came, we were kept in ward under the Law, shut up unto the faith which was to be revealed.
24 Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
So then the Law hath been our schoolmaster, to lead us to Christ, that we might be accepted as righteous through faith;
25 Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
but faith having come, we are no longer under a schoolmaster.
26 Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
For ye are all sons of God through faith in Christ Jesus;
27 Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
for as many of you as were baptized into Christ, did put on Christ.
28 Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
There is neither Jew nor Greek, there is neither bond nor free, there is no male and female; for ye are all one in Christ Jesus;
29 Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.
and if ye belong to Christ, then are ye Abraham's offspring, heirs according to the promise.

< Wagalatia 3 >