< Wagalatia 3 >
1 Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
O inconsiderate Galatians! who has deceived you, before whose eyes Jesus Christ crucified, was evidently represented among you?
2 Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
This, only, I wish to learn from you, did you receive the Spirit by works of law, or by obedience of faith?
3 Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
Are you so inconsiderate that, having begun in Spirit, you are now made perfect in flesh?
4 Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
Have you suffered so many things in vain? if, indeed, it is in vain?
5 Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
He, then, who ministered to you the Spirit, and wrought miracles among you, did he these by works of law, or by a hearing of faith?
6 Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
even as Abraham believed God, and it was counted to him for righteousness;
7 Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
know, therefore, that they who are of faith, the same are sons of Abraham.
8 Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
For the scripture, foreshowing that God would justify the nations by faith, formerly announced the gospel to Abraham, saying, "Surely in you shall all the nations be blessed."
9 Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
Wherefore, they who are of faith are blessed with believing Abraham.
10 Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
But as many as are of works of law, are under the curse: for it is written, "Accursed is every one who continues not in all things which are written in the book of the law, to do them."
11 Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
Besides, that by law no one is justified before God is manifest: "For the just by faith shall live."
12 Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
Now, the law is not of faith; but he who does these things, shall live by them.
13 Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
Christ has bought us off from the curse of the law, having become a curse for us: (for it is written, "Accursed is every one who is hanged on a tree": )
14 Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
that the blessing of Abraham might come on the nations through Christ Jesus; and that we might receive the promise of the Spirit through faith.
15 Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
Brethren, I speak after the manner of men: no one sets aside, or alters a man's Will, after it is ratified.
16 Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
Now, to Abraham were the promises spoken, and to his seed. He does not say, "And in seeds," as concerning many; but as concerning one person, "And in your see," who is Christ.
17 Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
Wherefore, this I affirm, that the Will which was before ratified by God concerning Christ, the law, which was made four hundred and thirty years after can not annul, so as to abolish the promise.
18 Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
Besides, if the inheritance be by law, it is no longer by promise. But God bestowed it freely on Abraham by promise.
19 Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
Why, then, the law? It was added on account of transgression, till the seed should come to whom it was promised; being ordained by messengers, in the hand of a Mediator;
20 Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
and the Mediator is not one party; but God is one party.
21 Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
Is the law, then, contrary to the promise of God? By no means. For if there had been a law given, which was able to make alive, certainly righteousness would have been by law.
22 Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
But the scripture has shut up together all under sin, that the promise by faith of Jesus Christ might be given to them that believe.
23 Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
Wherefore, before faith came, we were kept in durance under law, shut up together to the faith, which should afterward be revealed.
24 Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
So that the law has become our instructor to Christ, that we might be justified by faith.
25 Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
But faith being come, we are no longer under this instructor.
26 Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
For you are all the sons of God through the faith by Christ Jesus.
27 Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
Besides, as many of you have been immersed into Christ, have put on Christ.
28 Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
There is neither Jew nor Greek, there is neither bondman nor freeman, there is neither male nor female; for you are all one in Christ Jesus.
29 Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.
And if you are Christ's, certainly you are Abraham's seed, and heirs according to the promise.