< Wagalatia 3 >
1 Ninyi Wagalatia wajinga! Ni nani aliyewaroga? Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele yenu kwamba amesulubiwa.
O foolish Galatians! Who has bewitched you that you not be persuaded by the Truth—Jesus Christ was clearly portrayed among you as having been crucified, before your very eyes!
2 Nataka nijifunze neno moja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa kushika sheria, au kwa kuyaamini yale mliyosikia?
Just tell me one thing: Did you receive the Spirit by works of law, or by hearing of faith?
3 Je, ninyi ni wajinga kiasi hicho? Baada ya kuanza kwa Roho, je, sasa mwataka kumalizia katika mwili?
Can you be so foolish? Having begun in spirit, do you finish in flesh?
4 Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
Have you suffered so much for nothing—if it really was for nothing?
5 Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
Furthermore, He who supplies the Spirit to you and works miracles among you, is He activated by works of law, or by hearing of faith?—
6 Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
just as Abraham ‘believed God and it was credited to him as righteousness.’
7 Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
Now you must know that only those who are of faith are ‘sons’ of Abraham.
8 Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
Further, the Scripture, foreseeing that God would justify the nations by faith, proclaimed the Gospel in advance to Abraham: “All the nations will be blessed through you.”
9 Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
So then, those who are of faith are blessed along with Abraham, the faithful.
10 Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
Now as many as are ‘by works of law’ are under a curse; because it stands written, “Cursed is everyone who does not continue in all the things written in the Book of the Law, to do them.”
11 Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
Further, it is evident that no one is justified by law before God, because “the righteous one will live by faith.”
12 Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
While the law is not of faith but, “the man who does them will live by them.”
13 Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
Christ redeemed us from the curse of the law, having become a curse in our place—because it stands written, “Cursed is everyone who is hung on a tree”—
14 Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
so that the blessing of Abraham might come to the nations/Gentiles through Christ Jesus; that we might receive the promise of the Spirit through the faith.
15 Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
Brothers: as a man I speak a covenant; though only of a man, once it has been ratified no one annuls or adds to it.
16 Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
But to Abraham were spoken the promises, and to his Seed. He does not say “and to seeds,” as about many, but “and to your seed,” as about one, who is Christ.
17 Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
Further, I say this: a covenant confirmed beforehand by God in Christ cannot be annulled by the law that came four hundred and thirty years later, so as to make the promise of no effect.
18 Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
For if the inheritance were of law, it would no longer be of promise, but God granted it to Abraham by promise.
19 Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
Why then the law? It was added on account of the transgressions, until the Seed should come to whom the inheritance had been promised; and it was ordered through angels by the hand of a mediator.
20 Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
(Now that mediator is not for just one, but God is one.)
21 Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
Is the law then against the promises of God? Of course not! Rather, if a law had been given that was capable of imparting life, truly righteousness would have been by the law.
22 Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
But the Scripture imprisoned everything under sin, so that the promise by faith in Jesus Christ might be given to those who believe.
23 Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
Now before this faith came, we were kept in custody under the law, in confinement until the coming faith was revealed.
24 Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
So then, the law became our guardian until Christ, so that we might be justified by faith.
25 Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
Now that the faith has come, we are no longer under a guardian.
26 Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
So all of you are sons of God through the faith in Christ Jesus.
27 Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
As many of you as were baptized into Christ have clothed yourselves with Christ
28 Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.
—there is neither Jew nor Greek, there is neither slave nor free, there is no ‘male and female’; all of you are one in Christ Jesus—
29 Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.
so if you are Christ's, then you are Abraham's seed and heirs according to the promise.