< Wagalatia 2 >
1 Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
After that, fourteen years later, I, again, went up unto Jerusalem, with Barnabas, taking with me Titus also;
2 Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
And I went up by revelation, and laid before them the glad-message which I proclaim among the nations; privately, however, to them of repute, —lest, by any means, in vain, I should be running, or had run.
3 Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
But, not even Titus, who was with me, though he was a Greek, was compelled to be circumcised; —
4 Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
But, [this was] because of the false brethren secretly introduced, —who, indeed, came in secretly to spy out our freedom, which we have in Christ Jesus, that they might bring us into bondage: —
5 hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
Unto whom, not even for an hour, gave we place by the [required] submission, —in order that, the truth of the glad-message, might still abide with you.
6 Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote.
Moreover, from them who were reputed to be something, —whatsoever at one time, they were, maketh no difference to me, God accepteth not a man’s person, —unto me, in fact, they who were of repute added nothing further;
7 Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi.
But, on the contrary, —when they saw that I had been entrusted with the glad-message to the uncircumcision, even as, Peter, [with that] to the circumcision,
8 Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa.
For, he that energised in Peter, into an apostleship to the circumcision, energised also in me, for the nations, —
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi.
And when they perceived the favour which had been given unto me, James and Cephas and John, who were reputed to be pillars, gave, the right hand of fellowship, unto me and Barnabas, in order that, we, [should go] unto the nations, and, they, unto the circumcision: —
10 Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.
Only that we should remember, the destitute, —as to which I had given diligence, this very thing, to do.
11 Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpinga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosea kwa wazi.
But, when Cephas came unto Antioch, to the face, [even], him, I resisted, because he stood condemned;
12 Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu wa Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
For, before that certain came from James, with them of the nations, used he to eat; whereas, when they came, he used to withdraw, and keep himself separate, fearing them of the circumcision;
13 Pia Wayahudi wengine waliungana naye katika unafiki huu, hata Barnaba naye akapotoshwa na unafiki wao.
And the rest of the Jews [also] used hypocrisy with him, so that, even Barnabas, was carried away by their hypocrisy.
14 Nilipoona kwamba hawatendi sawasawa na kweli ya Injili, nilimwambia Petro mbele ya wote, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu wa Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?
But, when I saw that they were not walking with straightforwardness as regardeth the truth of the glad-message, I said unto Cephas, before all: If, thou, although, a Jew, like them of the nations, and not like the Jews, dost live, how dost thou compel, them of the nations, to live like Jews?
15 “Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,
We, by nature Jews, and not sinners from among the nations,
16 bado tunajua ya kwamba mtu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hivyo sisi pia, tumemwamini Kristo Yesu ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Kristo, wala si kwa matendo ya sheria, kwa sababu kwa kushika sheria hakuna hata mtu mmoja atakayehesabiwa haki.
Knowing, however, that a man is not declared righteous by works of law, [nor at all] save through faith in Christ Jesus; even we, on Christ Jesus, believed, that we might be declared righteous—by faith in Christ, and not by works of law; because, by works of law, shall no flesh be declared righteous.
17 “Lakini tukitafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, inakuwa dhahiri kwamba sisi ni wenye dhambi. Je, ina maana kwamba Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!
Now, if in seeking to be declared righteous in Christ we, ourselves also, were found sinners, —is Christ, therefore, a minister, of sin? Far be it!
18 Lakini ikiwa mimi ninajenga tena kile ambacho nimekwisha kukibomoa, basi ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji.
For, if, the things that I pulled down, these, again, I build, a transgressor, I prove, myself, to be.
19 Kwa maana mimi kwa njia ya sheria, nimeifia sheria ili nipate kuishi kwa ajili ya Mungu.
For, I, through means of law, unto law, died, that, unto God, I might live: —
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu.
With Christ, have I been crucified; and, living no longer, am, I, but, living in me, is, Christ, —while, so far as I now do live in flesh, by faith, I live—The faith in the Son of God, who loved me, and gave himself up in my behalf.
21 Siibatilishi neema ya Mungu, kwa maana kama haki ingeweza kupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure!”
I do not set aside the favour of God; for, if, through law, is righteousness, then, Christ, without cause, died.