< Wagalatia 2 >
1 Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
Fourteen years afterward I went up to Jerusalem again with Barnabas, and I took Titus also with me.
2 Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
It was in obedience to a revelation that I went; and I laid before the apostles the good news that I am proclaiming among the Gentiles. I did this privately before those who are thought highly of because I was afraid that I might possibly be taking, or might have already taken, a course which would prove useless.
3 Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
Yet even my companion, Titus, though a Greek, was not compelled to be circumcised.
4 Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
But, because of those who pretended to be followers who had stolen in, the intruders who had crept in to spy on the liberty which we have through union with Christ Jesus, in order to bring us back to slavery –
5 hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
Why, we did not for a moment yield submission to them, so that the truth of the good news might be yours always!
6 Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote.
Of those who are thought somewhat highly of – what they once were makes no difference to me; God does not recognize human distinctions – those, I say, who are thought highly of added nothing to my message.
7 Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi.
On the contrary, they saw that I had been entrusted with the good news for the Gentiles, just as Peter had been for the Jews.
8 Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa.
For he who gave Peter power for his mission to the Jews gave me, also, power to go to the Gentiles.
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi.
Recognizing the charge entrusted to me, James, Peter, and John, who were regarded as pillars of the church, openly acknowledged Barnabas and me as fellow workers, agreeing that we should go to the Gentiles, and they to the Jews.
10 Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.
Only we were to remember the poor – the thing I was myself anxious to do.
11 Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpinga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosea kwa wazi.
But, when Peter came to Antioch, I opposed him to his face; for he stood self-condemned.
12 Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu wa Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
Before certain persons came from James, he had been in the habit of eating with the Gentile converts; but, when they came, he began to withdraw and hold aloof, because he was afraid of offending those who still held to circumcision.
13 Pia Wayahudi wengine waliungana naye katika unafiki huu, hata Barnaba naye akapotoshwa na unafiki wao.
The rest of the Jewish converts were guilty of the same hypocrisy, so that even Barnabas was led away by it.
14 Nilipoona kwamba hawatendi sawasawa na kweli ya Injili, nilimwambia Petro mbele ya wote, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu wa Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?
But, when I saw that they were not dealing straightforwardly with the truth of the good news, I said to Peter, before them all, “If you, who were born a Jew, adopt Gentile customs, instead of Jewish, why are you trying to compel the Gentile converts to adopt Jewish customs?”
15 “Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,
We, though we are Jews by birth and not sinners of Gentile origin, know that no one is pronounced righteous as the result of obedience to Law, but only through faith in Christ Jesus.
16 bado tunajua ya kwamba mtu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hivyo sisi pia, tumemwamini Kristo Yesu ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Kristo, wala si kwa matendo ya sheria, kwa sababu kwa kushika sheria hakuna hata mtu mmoja atakayehesabiwa haki.
So we placed our faith in Christ Jesus, in order that we might be pronounced righteous, as the result of faith in Christ, and not of obedience to Law; for such obedience will not result in even one soul’s being pronounced righteous.
17 “Lakini tukitafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, inakuwa dhahiri kwamba sisi ni wenye dhambi. Je, ina maana kwamba Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!
If, while seeking to be pronounced righteous through union with Christ, we were ourselves seen to be sinners, would that make Christ an agent of sin? Heaven forbid!
18 Lakini ikiwa mimi ninajenga tena kile ambacho nimekwisha kukibomoa, basi ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji.
For, if I rebuild the things that I pulled down, I prove myself to have done wrong.
19 Kwa maana mimi kwa njia ya sheria, nimeifia sheria ili nipate kuishi kwa ajili ya Mungu.
I, indeed, through Law became dead to Law, in order to live for God.
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu.
I have been crucified with Christ. So it is no longer I that live, but it is Christ who lives in me; and, as for my present earthly life, I am living it by faith in the Son of God, who loved me and gave himself for me.
21 Siibatilishi neema ya Mungu, kwa maana kama haki ingeweza kupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure!”
I do not reject the love of God. If righteousness comes through Law, then there was no need for Christ to die!