< Wagalatia 2 >

1 Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
Then, fourteen years after, I went up again to Jerusalem with Barnabas, and took Titus also with me.
2 Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
And I went up by revelation, and communicated to them that gospel which I preach among the gentiles; but privately to those who were of reputation, lest by any means I should run, or had run, in vain.
3 Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
But not even Titus, who was with me, though he was a Greek, was compelled to be circumcised;
4 Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
and that because of the false brethren stealthily brought in, who crept in to spy out our liberty which we have in Christ Jesus, that they might bring into bondage;
5 hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
to whom not even for an hour did we yield by the required subjection, that the truth of the gospel might still remain with you.
6 Kwa habari ya wale waliokuwa wakubaliwe kuwa viongozi (kwangu mimi sikujali vyeo vyao, maana Mungu hana upendeleo), wale watu hawakuniongezea chochote.
But from those who were reputed to be somewhat—whatever they were, it matters not to me, (God accepteth no man's person, ) for to me those in reputation communicated nothing new.
7 Badala yake walitambua kwamba nilikuwa nimekabidhiwa kazi ya kuhubiri Injili kwa watu wa Mataifa, kama vile Petro alivyokabidhiwa kuhubiri Injili kwa Wayahudi.
But on the contrary, when they saw that I was intrusted with the gospel to the uncircumcised, as Peter was with that to the circumcised,
8 Kwa maana, Mungu aliyekuwa akitenda kazi katika huduma ya Petro kama mtume kwa Wayahudi, ndiye pia aliyekuwa anatenda kazi katika huduma yangu kama mtume kwa watu wa Mataifa.
(for he who wrought for Peter in behalf of the apostleship to the circumcised, wrought also for me in behalf of the gentiles, )
9 Basi, Yakobo, Kefa na Yohana, walioonekana kama nguzo za kanisa, walitupa mkono wa shirika, mimi na Barnaba walipotambua ile neema niliyopewa. Wakakubali kwamba sisi twende kwa watu wa Mataifa na wao waende kwa Wayahudi.
and when they knew the grace that was given to me, James and Cephas and John, who were reputed to be pillars, gave to me and Barnabas the right hand of fellowship, that we should go to the gentiles, and they to the circumcised;
10 Walichotuomba ni kwamba tuendelee kuwakumbuka maskini, jambo ambalo ndilo nililokuwa na shauku ya kulifanya.
only they wished us to remember the poor; which very thing I also was earnest to do.
11 Lakini Petro alipofika Antiokia, mimi nilimpinga ana kwa ana kwa sababu alikuwa amekosea kwa wazi.
But when Cephas came to Antioch, I withstood him to the face; for he was condemned.
12 Kabla baadhi ya watu waliotoka kwa Yakobo hawajafika, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa. Lakini hao watu walipofika alianza kujiondoa na kujitenga na watu wa Mataifa kwa sababu aliwaogopa wale wa kundi la tohara.
For before certain persons came from James, he used to eat with the gentiles; but when they came, he withdrew, and separated himself, fearing those who were of the circumcision.
13 Pia Wayahudi wengine waliungana naye katika unafiki huu, hata Barnaba naye akapotoshwa na unafiki wao.
And the other Jews also dissembled with him; so that even Barnabas was carried away with their dissimulation.
14 Nilipoona kwamba hawatendi sawasawa na kweli ya Injili, nilimwambia Petro mbele ya wote, “Wewe ni Myahudi, nawe unaishi kama mtu wa Mataifa na wala si kama Myahudi. Imekuwaje basi, mnawalazimisha watu wa Mataifa kufuata desturi za Kiyahudi?
But when I saw that they were not walking uprightly according to the truth of the gospel, I said to Cephas in the presence of all, If thou, being a Jew, livest after the manner of gentiles, and not that of the Jews, how is it that thou compellest the gentiles to keep the customs of the Jews?
15 “Sisi wenyewe ni Wayahudi kwa kuzaliwa na si watu wenye dhambi kama watu wa Mataifa,
We are Jews by nature, and not sinners of the gentiles;
16 bado tunajua ya kwamba mtu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria bali kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Hivyo sisi pia, tumemwamini Kristo Yesu ili tupate kuhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Kristo, wala si kwa matendo ya sheria, kwa sababu kwa kushika sheria hakuna hata mtu mmoja atakayehesabiwa haki.
but knowing that a man is not accepted as righteous by the works of the Law, but by faith in Christ Jesus, we also have believed in Christ Jesus, that we might be accepted as righteous by faith in Christ, and not by the works of the Law; for by the works of the Law shall no flesh be accepted as righteous.
17 “Lakini tukitafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, inakuwa dhahiri kwamba sisi ni wenye dhambi. Je, ina maana kwamba Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? La hasha!
But while seeking to be accepted as righteous in Christ, we ourselves also are found sinners, is Christ therefore a minister of sin? Far be it!
18 Lakini ikiwa mimi ninajenga tena kile ambacho nimekwisha kukibomoa, basi ninaonyesha kwamba mimi ni mkosaji.
For if I again build up what I pulled down, I make myself a transgressor.
19 Kwa maana mimi kwa njia ya sheria, nimeifia sheria ili nipate kuishi kwa ajili ya Mungu.
For I through the Law died to the Law, that I might live to God.
20 Nimesulubiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi, bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu.
I have been crucified with Christ, and no longer do I live, but Christ liveth in me; and the life which I now live in the flesh I live in faith in the Son of God, who loved me, and gave himself for me.
21 Siibatilishi neema ya Mungu, kwa maana kama haki ingeweza kupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure!”
I do not set aside the grace of God; for if righteousness come through the Law, then did Christ die for nought.

< Wagalatia 2 >