< Wagalatia 1 >
1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paweł, Apostoł (nie od ludzi, ani przez człowieka, ale przez Jezusa Chrystusa i Boga Ojca, który go wzbudził od umarłych; )
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
I wszyscy bracia, którzy są ze mną, zborom Galackim.
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Łaska wam i pokój niech będzie od Boga Ojca i Pana naszego, Jezusa Chrystusa.
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn )
Który wydał samego siebie za grzechy nasze, aby nas wyrwał z teraźniejszego wieku złego według woli Boga i Ojca naszego; (aiōn )
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
Któremu niech będzie chwała na wieki wieków. Amen. (aiōn )
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
Dziwuję się, iż tak prędko dacie się przenosić od tego, który was powołał ku łasce Chrystusowej, do inszej Ewangielii;
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
Która nie jest inszą; tylko niektórzy są, co was turbują i chcą wywrócić Ewangieliję Chrystusową.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
Ale choćbyśmy i my, albo Anioł z nieba opowiadał wam Ewangieliję mimo tę, którąśmy wam opowiadali, niech będzie przeklęty.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
Jakośmy przedtem powiedzieli i teraz znowu mówię: Jeźliby wam kto inną Ewangieliję opowiadał mimo tę, którąście przyjęli, niech będzie przeklęty.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
Albowiem terazże do ludzi was namawiam, czyli do Boga? Albo szukamli, abym się podobał ludziom? Zaiste, jeźlibym się jeszcze ludziom chciał podobać, nie byłbym sługą Chrystusowym.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
A oznajmuję wam bracia! iż Ewangielija, która jest opowiadana ode mnie, nie jest według człowieka.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
Albowiem ja anim jej wziął, anim się jej nauczył od człowieka, ale przez objawienie Jezusa Chrystusa.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
Boście słyszeli o mojem obcowaniu niekiedy w Żydostwie, żem nader prześladował zbór Boży i burzyłem go;
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
I postępowałem w Żydostwie nad wiele rówieśników moich w narodzie moim, będąc nader gorliwym miłośnikiem ustaw moich ojczystych.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
Ale gdy się upodobało Bogu, który mię odłączył z żywota matki mojej, i powołał z łaski swojej,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
Aby objawił Syna swego we mnie, abym go opowiadał między poganami, wnetże nie radziłem się ciała i krwi;
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
Anim się wrócił do Jeruzalemu, do tych, którzy przede mną byli Apostołami, alem szedł do Arabii i wróciłem się zasię do Damaszku.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Potem po trzech latach wstąpiłem do Jeruzalemu, abym się ujrzał z Piotrem; i mieszkałem u niego piętnaście dni.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
A inszegom z Apostołów nie widział, oprócz Jakóba, brata Pańskiego.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
A co wam piszę, oto się przed Bogiem oświadczam, żeć nie kłamię.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Zatemem przyszedł do krain Syryi i Cylicyi;
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
A byłem nieznajomym z twarzy zborom żydowskim, które są w Chrystusie;
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
Lecz tylko byli usłyszeli, iż ten, który prześladował nas niekiedy, teraz opowiada wiarę, którą przedtem burzył.
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
I chwalili Boga ze mnie.