< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an apostle—not an apostle from men nor by human agency, but through Jesus Christ and God the Father, who raised him from the dead—
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brothers with me, to the churches of Galatia:
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave himself for our sins so that he might deliver us from this present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to him be the glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I am amazed that you are turning away so quickly from him who called you by the grace of Christ. I am amazed that you are turning to a different gospel.
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
This is not to say that there is another gospel, but there are some men who cause you trouble and want to change the gospel of Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But even if we or an angel from heaven should proclaim to you a gospel other than the one we proclaimed to you, let him be cursed.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have said before, so now I say again, “If someone proclaims to you a gospel other than the one you received, let him be cursed.”
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For am I now seeking the approval of men or God? Am I seeking to please men? If I am still trying to please men, I am not a servant of Christ.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
For I want you to know, brothers, that the gospel I proclaimed is not man's gospel.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
I did not receive it from any man, nor was I taught it. Instead, it was by revelation of Jesus Christ to me.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
You have heard about my former life in Judaism, how I was persecuting the church of God beyond measure and that I was trying to destroy it.
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
I advanced in Judaism beyond many of those who were my own age, from out of my own people. That is how extremely zealous I was for the traditions of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when God, who had set me apart from my mother's womb, and who called me through his grace,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
was pleased to reveal his Son in me, so that I would proclaim him among the Gentiles, I did not immediately consult with flesh and blood.
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
I did not go up to Jerusalem to those who had become apostles before me. Instead, I went to Arabia and then returned to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then after three years I went up to Jerusalem to get to know Cephas and I stayed with him fifteen days.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
But I saw none of the other apostles except James, the Lord's brother.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
In what I write to you, I assure you before God, that I am not lying.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Then I went to the regions of Syria and Cilicia.
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
I was still not personally known to the churches of Judea that are in Christ.
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
They only heard it being said, “The man who once persecuted us is now proclaiming the faith he once tried to destroy.”
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
So they glorified God because of me.

< Wagalatia 1 >