< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an apostle, not from men, nor through man, but through Jesus Christ, and God the Father, who raised him from the dead, —
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren that are with me, to the churches of Galatia:
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Grace be to you and peace from God the Father, and from our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave himself for our sins, that he might deliver us from the present evil world, according to the will of God our Father; (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to whom be the glory for ever and ever! Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I marvel that ye are so soon turning from him that called you in the grace of Christ, to a different gospel;
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
which is not another; only there are certain persons who are troubling you, and seeking to change entirely the gospel of Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But even if we or an angel from heaven should preach a gospel to you contrary to that which we preached to you, let him be accursed!
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have said before, so I now say again, If any one preach a gospel to you contrary to that which ye received, let him be accursed!
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For do I now seek the favor of men, or of God? Or am I endeavoring to please men? If I were still pleasing men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
But I assure you, brethren, that the gospel which was preached by me is not after man;
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
for I did not receive it from man nor was I taught it by any man, but it was revealed to me by Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For ye have heard of my conduct formerly in Judaism; that beyond measure I persecuted the church of God, and was destroying it,
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and made progress in Judaism beyond many of the same age with me in my nation, being more exceedingly zealous for the traditions of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when it pleased him who set me apart from my very birth, and called me through his grace,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
to reveal his Son within me, that I might publish the glad tidings of him among the gentiles, immediately I conferred not with flesh and blood,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
neither did I go up to Jerusalem to those who were apostles before me, but I went away into Arabia, and returned again to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then, after three years, I went up to Jerusalem to become acquainted with Cephas, and stayed with him fifteen days;
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
but no other of the apostles did I see, save James the brother of the Lord.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Now as to what I am writing to you, behold, before God, I do not lie.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Afterwards I came into the regions of Syria and Cilicia;
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
and I was unknown by face to the churches of Judaea which were in Christ;
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
but they were only hearing that “He who was once our persecutor is now preaching the faith which he was once destroying”;
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
and they glorified God in me.

< Wagalatia 1 >