< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
PAUL the apostle (not sent from men, nor by man, but by Jesus Christ, and our Father who raised him from the dead),
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren with me, to the churches of Galatia:
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
grace unto you, and peace from God the Father and our Lord Jesus Christ;
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave himself for our sins, that he might pluck us out of this present wicked world, according to the will of God and our Father: (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to whom be glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I marvel that ye are so quickly departed from him that called you, by the grace of Christ into another gospel
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
which is not another; but there are certain persons who trouble you, and desire to pervert the gospel of Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But though even we, or an angel from heaven, preach unto you another gospel, different from that which we have preached to you, let him be an anathema.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have before spoken, and I now repeat it again, If any man preach a gospel different from that ye have received, let him be anathema.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For do I now use persuasions from men, or from God? or do I seek to please men? for if I yet pleased men, I should not be the servant of Christ.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
But I give you to understand, brethren, that the gospel which was preached by me is not a merely human ministry.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
For I neither received it from man, nor was taught, but by immediate revelation from Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For ye have heard of my former manner of life, when I professed Judaism, that in the most outrageous manner I persecuted the church of God, and wasted it:
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and signalized myself in Judaism above many of those of my own age among my countrymen, being more exceedingly a zealot for the traditions of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when it pleased God, who selected me from my mother’s womb, and called me by his grace,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
to reveal his Son in me, that I might preach the glad tidings of him to the nations, immediately I conferred not with flesh and blood,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
nor went up to Jerusalem to those who were apostles before me; but I went away into Arabia, and returned again unto Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Afterwards at the expiration of three years I went up unto Jerusalem to pay a visit to Peter, and I abode with him fifteen days.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
But I saw no other of the apostles except James, the Lord’s brother.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Now respecting the things which I write unto you, behold, in the presence of God, I lie not.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Afterwards I went into the regions of Syria and Cilicia;
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
and I was personally unknown to the churches of Judea, which are in Christ:
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
only they had heard, that he who persecuted us in time past, now preaches the faith which he once laid waste.
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
And they glorified God on my behalf.

< Wagalatia 1 >