< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, apostle, not from men nor through man, but through Jesus Christ, and God [the] Father who raised him from among [the] dead,
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
and all the brethren with me, to the assemblies of Galatia.
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Grace to you, and peace, from God [the] Father, and our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
who gave himself for our sins, so that he should deliver us out of the present evil world, according to the will of our God and Father; (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
to whom [be] glory to the ages of ages. Amen. (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I wonder that ye thus quickly change, from him that called you in Christ's grace, to a different gospel,
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
which is not another [one]; but there are some that trouble you, and desire to pervert the glad tidings of the Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But if even we or an angel out of heaven announce as glad tidings to you [anything] besides what we have announced as glad tidings to you, let him be accursed.
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have said before, now also again I say, If any one announce to you as glad tidings [anything] besides what ye have received, let him be accursed.
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For do I now seek to satisfy men or God? or do I seek to please men? If I were yet pleasing men, I were not Christ's bondman.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
But I let you know, brethren, [as to] the glad tidings which were announced by me, that they are not according to man.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
For neither did I receive them from man, neither was I taught [them], but by revelation of Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For ye have heard [what was] my conversation formerly in Judaism, that I excessively persecuted the assembly of God, and ravaged it;
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
and advanced in Judaism beyond many [my] contemporaries in my nation, being exceedingly zealous of the doctrines of my fathers.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But when God, who set me apart [even] from my mother's womb, and called [me] by his grace,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
was pleased to reveal his Son in me, that I may announce him as glad tidings among the nations, immediately I took not counsel with flesh and blood,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
nor went I up to Jerusalem to those [who were] apostles before me; but I went to Arabia, and again returned to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then after three years I went up to Jerusalem to make acquaintance with Peter, and I remained with him fifteen days;
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
but I saw none other of the apostles, but James the brother of the Lord.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Now what I write to you, behold, before God, I do not lie.
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
Then I came into the regions of Syria and Cilicia.
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
But I was unknown personally to the assemblies of Judaea which [are] in Christ;
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
only they were hearing that he who persecuted us formerly now announces the glad tidings of the faith which formerly he ravaged:
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
and they glorified God in me.

< Wagalatia 1 >