< Ezra 1 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Bwana lililosemwa na nabii Yeremia, Bwana aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:
En la première année de Cyrus, roi des Perses, afin que fût accomplie la parole du Seigneur, annoncée par la bouche de Jérémie, le Seigneur suscita l’esprit de Cyrus, roi des Perses, et fit publier dans tout son royaume un édit, même par écrit, disant:
2 “Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi: “‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda.
Voici ce que dit Cyrus, roi des Perses: Le Seigneur Dieu du ciel m’a donné tous les royaumes de la terre, et lui-même m’a ordonné de lui bâtir une maison à Jérusalem, qui est dans la Judée.
3 Yeyote wa watu wake miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha apande kwenda Yerusalemu katika Yuda na kujenga Hekalu la Bwana, Mungu wa Israeli, Mungu aliyeko huko Yerusalemu.
Qui est parmi vous de tout son peuple? Que son Dieu soit avec lui; qu’il monte à Jérusalem, qui est en Judée, et qu’il bâtisse la maison du Seigneur Dieu d’Israël; c’est le Dieu qui est à Jérusalem;
4 Nao watu wa mahali popote wale walionusurika wanapoishi sasa, watu hao wampe fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, mbali na sadaka za hiari kwa ajili ya Hekalu la Mungu huko Yerusalemu.’”
Et que tous les autres, dans tous les lieux où ils habitent, les hommes de son lieu, l’aident en argent, en or, en biens et en troupeaux, outre ce qu’ils offrent volontairement au temple de Dieu qui est à Jérusalem.
5 Kisha viongozi wa jamaa ya Yuda na Benyamini na makuhani na Walawi kila mmoja ambaye moyo wake ulisukumwa na Mungu, akajiandaa kupanda ili kuijenga nyumba ya Bwana huko Yerusalemu.
Alors se levèrent les princes des pères de Juda et de Benjamin, les prêtres, les Lévites, et tous ceux dont Dieu suscita l’esprit, pour monter afin de bâtir le temple du Seigneur qui était à Jérusalem.
6 Majirani zao wote wakawasaidia vyombo vya fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, pia na zawadi za thamani, pamoja na sadaka zote za hiari.
Et tous ceux qui étaient dans les environs mirent en leurs mains des vases d’argent et d’or, les biens, les troupeaux, et les meubles, outre ce qu’ils avaient spontanément offert.
7 Zaidi ya hayo, Mfalme Koreshi akavitoa vyombo vilivyokuwa mali ya Hekalu la Bwana, ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka Yerusalemu na kuviweka katika hekalu la mungu wake.
Le roi Cyrus remit aussi les vases du temple du Seigneur, que Nabuchodonosor avait emportés de Jérusalem, et qu’il avait mis dans le temple de son dieu.
8 Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa kwa mkono wa Mithredathi mtunza hazina, aliyevihesabu mbele ya Sheshbaza mkuu wa Yuda.
Or Cyrus, roi des Perses, les rendit par l’entremise de Mithridate, fils de Gazabar, et les compta à Sassabasar, prince de Juda.
9 Hii ilikuwa ndio orodha ya vifaa: masinia ya dhahabu yalikuwa 30 masinia ya fedha yalikuwa 1,000 vyetezo vya fedha vilikuwa 29
Et en voici le nombre: Trente fioles d’or, mille fioles d’argent, vingt-neuf couteaux, trente coupes d’or;
10 mabakuli ya dhahabu yalikuwa 30 mabakuli ya fedha yanayofanana yalikuwa 410 vifaa vingine vilikuwa 1,000.
Quatre cent dix coupes d’argent du second ordre; mille autres vases.
11 Kwa ujumla, kulikuwa na vyombo 5,400 vya dhahabu na vya fedha. Sheshbaza akavileta hivi vyote wakati watu walipotoka uhamishoni Babeli kwenda Yerusalemu.
Tous les vases d’or et d’argent, cinq mille quatre cents: Sassabasar les remporta tous avec les Juifs qui montaient de la transmigration de Babylone à Jérusalem.

< Ezra 1 >