< Ezra 1 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Bwana lililosemwa na nabii Yeremia, Bwana aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:
La première année de la domination de Cyrus, roi des Perses, la parole du Seigneur qu'avait proférée la bouche de Jérémie le prophète, devait s'accomplir; le Seigneur excita l'esprit de Cyrus, roi des Perses, et il envoya en tout son royaume une proclamation par écrit, disant:
2 “Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi: “‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda.
Voici ce qu'a dit Cyrus, roi des Perses: Le Seigneur Dieu du ciel m'a donné tous les royaumes de la terre, et lui-même a jeté les yeux sur moi pour que je lui bâtisse un temple à Jérusalem en Judée.
3 Yeyote wa watu wake miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha apande kwenda Yerusalemu katika Yuda na kujenga Hekalu la Bwana, Mungu wa Israeli, Mungu aliyeko huko Yerusalemu.
Qui donc, parmi vous tous, est de son peuple? Son Dieu sera avec lui, et il partira pour Jérusalem en Judée; qu'il y bâtisse le temple du Dieu d'Israël; le seul Dieu est celui qui réside à Jérusalem.
4 Nao watu wa mahali popote wale walionusurika wanapoishi sasa, watu hao wampe fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, mbali na sadaka za hiari kwa ajili ya Hekalu la Mungu huko Yerusalemu.’”
Tous ceux de ce peuple qui vivent encore, en quelque lieu qu'ils habitent, les hommes de ce lieu les aideront de dons en argent, en or, en meubles, ou en bestiaux, outre ce qu'ils offriront volontairement pour le temple de Dieu à Jérusalem.
5 Kisha viongozi wa jamaa ya Yuda na Benyamini na makuhani na Walawi kila mmoja ambaye moyo wake ulisukumwa na Mungu, akajiandaa kupanda ili kuijenga nyumba ya Bwana huko Yerusalemu.
Alors, se levèrent les chefs de famille de Juda et de Benjamin, et les prêtres et les lévites, tous ceux que l'Esprit de Dieu excita à partir et à relever le temple du Seigneur à Jérusalem.
6 Majirani zao wote wakawasaidia vyombo vya fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, pia na zawadi za thamani, pamoja na sadaka zote za hiari.
Et tous ceux qui les entouraient leur fortifièrent les mains avec des vases d'argent, de l'or, des meubles, des bestiaux et des présents, outre les dons volontaires pour le temple.
7 Zaidi ya hayo, Mfalme Koreshi akavitoa vyombo vilivyokuwa mali ya Hekalu la Bwana, ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka Yerusalemu na kuviweka katika hekalu la mungu wake.
Et le roi Cyrus offrit les vases du temple du Seigneur que Nabuchodonosor avait enlevés de Jérusalem, et qu'il avait dédiés au temple de son Dieu.
8 Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa kwa mkono wa Mithredathi mtunza hazina, aliyevihesabu mbele ya Sheshbaza mkuu wa Yuda.
Cyrus, roi des Perses, les donna par la main de Mithradate le trésorier, et celui-ci les compta avec Sasabasar, chef de Juda.
9 Hii ilikuwa ndio orodha ya vifaa: masinia ya dhahabu yalikuwa 30 masinia ya fedha yalikuwa 1,000 vyetezo vya fedha vilikuwa 29
En voici le nombre: trente coupes d'or, mille d'argent, vingt-neuf de divers genres, trente coupes d'or,
10 mabakuli ya dhahabu yalikuwa 30 mabakuli ya fedha yanayofanana yalikuwa 410 vifaa vingine vilikuwa 1,000.
Quatre cent dix doubles coupes d'argent, et mille autres vases.
11 Kwa ujumla, kulikuwa na vyombo 5,400 vya dhahabu na vya fedha. Sheshbaza akavileta hivi vyote wakati watu walipotoka uhamishoni Babeli kwenda Yerusalemu.
Il y avait en tout cinq mille quatre cents vases d'or et d'argent qui furent emportés par Sasabasar, du lieu d'exil de Babylone, à Jérusalem.

< Ezra 1 >