< Ezra 1 >
1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Bwana lililosemwa na nabii Yeremia, Bwana aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:
In the first year of Cyrus, king of Persia, Yahweh fulfilled his word that came from the mouth of Jeremiah, and stirred Cyrus's spirit. Cyrus' voice went out over his entire kingdom. This is what was written and spoken:
2 “Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi: “‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda.
“Cyrus, king of Persia, says: Yahweh, God of Heaven, gave me all the kingdoms of the earth, and he appointed me to build for him a house in Jerusalem in Judea.
3 Yeyote wa watu wake miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha apande kwenda Yerusalemu katika Yuda na kujenga Hekalu la Bwana, Mungu wa Israeli, Mungu aliyeko huko Yerusalemu.
Whoever is from his people (may his God be with him) may go up to Jerusalem and build a house for Yahweh, the God of Israel, the God who is in Jerusalem.
4 Nao watu wa mahali popote wale walionusurika wanapoishi sasa, watu hao wampe fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, mbali na sadaka za hiari kwa ajili ya Hekalu la Mungu huko Yerusalemu.’”
People of any part of the kingdom where survivors of that land are living should provide them with silver and gold, possessions and animals, as well as a freewill offering for God's house in Jerusalem.”
5 Kisha viongozi wa jamaa ya Yuda na Benyamini na makuhani na Walawi kila mmoja ambaye moyo wake ulisukumwa na Mungu, akajiandaa kupanda ili kuijenga nyumba ya Bwana huko Yerusalemu.
Then the heads of the ancestors' clans of Judah and Benjamin, the priests and Levites, and everyone whose spirit God stirred to go and build his house arose.
6 Majirani zao wote wakawasaidia vyombo vya fedha na dhahabu, pamoja na vifaa na mifugo, pia na zawadi za thamani, pamoja na sadaka zote za hiari.
Those around them supported their work with silver and gold objects, possessions, animals, valuables, and freewill offerings.
7 Zaidi ya hayo, Mfalme Koreshi akavitoa vyombo vilivyokuwa mali ya Hekalu la Bwana, ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua kutoka Yerusalemu na kuviweka katika hekalu la mungu wake.
Cyrus king of Persia also released the objects belonging to Yahweh's house that Nebuchadnezzar had brought from Jerusalem and put in his own gods' houses.
8 Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa kwa mkono wa Mithredathi mtunza hazina, aliyevihesabu mbele ya Sheshbaza mkuu wa Yuda.
Cyrus put them into the hand of Mithredath the treasurer, who counted them out for Sheshbazzar, Judea's leader.
9 Hii ilikuwa ndio orodha ya vifaa: masinia ya dhahabu yalikuwa 30 masinia ya fedha yalikuwa 1,000 vyetezo vya fedha vilikuwa 29
This was their number: thirty gold basins, one thousand silver basins, twenty-nine other basins,
10 mabakuli ya dhahabu yalikuwa 30 mabakuli ya fedha yanayofanana yalikuwa 410 vifaa vingine vilikuwa 1,000.
thirty gold bowls, 410 small silver bowls, and one thousand additional objects.
11 Kwa ujumla, kulikuwa na vyombo 5,400 vya dhahabu na vya fedha. Sheshbaza akavileta hivi vyote wakati watu walipotoka uhamishoni Babeli kwenda Yerusalemu.
There were 5,400 gold and silver items in all. Sheshbazzar brought all of them when the exiles went from Babylon to Jerusalem.