< Ezra 9 >

1 Baada ya mambo haya kutendeka, viongozi walinijia na kusema, “Watu wa Israeli, wakiwemo makuhani na Walawi, hawakujitenga na majirani zao katika kufanya machukizo, kama yale ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri na Waamori.
Or sitôt que ces choses-là furent achevées, les principaux du peuple s'approchèrent vers moi, en disant: Le peuple d'Israël, et les Sacrificateurs, et les Lévites ne se sont point séparés des peuples de ces pays, [comme ils le devaient faire] à cause de leurs abominations, [savoir] des Cananéens, des Héthiens, des Phéréziens, des Jébusiens, des Hammonites, des Moabites, des Egyptiens, et des Amorrhéens.
2 Wamewaoa baadhi ya binti zao kuwa wake zao na wake za wana wao, nao wamechanganya taifa takatifu na watu waliowazunguka. Nao viongozi na maafisa wamekuwa mstari wa mbele katika njia hii potovu.”
Car ils ont pris de leurs filles pour eux et pour leurs fils; et la semence sainte a été mêlée avec les peuples de ces pays; et même il y a des principaux du peuple, et [plusieurs] magistrats, qui ont été les premiers à commettre ce péché.
3 Niliposikia jambo hili nilirarua koti langu na joho langu, nikazingʼoa nywele za kichwa changu na ndevu zangu na kuketi nikishangaa.
Et sitôt que j'eus entendu cela, je déchirai mes vêtements, et mon manteau, et j'arrachai les cheveux de ma tête, et [les poils] de ma barbe, et je m'assis tout désolé.
4 Kisha kila mmoja aliyetetemeshwa na maneno ya Mungu wa Israeli alikusanyika kunizunguka kwa sababu ya upotovu huu wa hao watu waliorudi kutoka utumwani. Nami niliketi pale nikishangaa mpaka wakati wa dhabihu ya jioni.
Et tous ceux qui tremblaient aux paroles du Dieu d'Israël, s'assemblèrent vers moi à cause du crime de ceux de la captivité, et je demeurai assis tout désolé jusqu'à l'oblation du soir.
5 Ndipo wakati wa kutoa dhabihu ya jioni nikainuka kutoka kujidhili kwangu nikiwa na koti na joho langu lililoraruka, nikapiga magoti mikono yangu ikiwa imeinuliwa kwa Bwana Mungu wangu.
Et au temps de l'oblation du soir je me levai de mon affliction, et ayant mes vêtements et mon manteau déchirés, je me mis à genoux, et j'étendis mes mains vers l'Eternel mon Dieu,
6 Nami nikaomba: “Ee Mungu wangu, natahayari na kuona aibu kukuinulia uso wangu Mungu wangu, kwa sababu dhambi zetu zimejikusanya hata kupita juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imefika mbinguni.
Et je dis: Mon Dieu! j'ai honte, et je suis trop confus pour [oser] élever, ô mon Dieu! ma face vers toi; car nos iniquités sont multipliées au dessus de nos têtes, et notre crime s'est élevé jusques aux cieux.
7 Tokea siku za babu zetu mpaka sasa, hatia yetu imekuwa kubwa. Kwa sababu ya dhambi zetu, sisi na wafalme wetu na makuhani wetu tumekabiliwa na vita, utumwa, kutekwa na kudhiliwa katika mikono ya wafalme wa kigeni, kama ilivyo leo.
Depuis les jours de nos pères jusqu'à aujourd'hui nous sommes extrêmement coupables; et nous avons été livrés à cause de nos iniquités, nous, nos Rois, et nos Sacrificateurs, entre les mains des Rois des pays, pour être mis au fil de l'épée, emmenés captifs, pillés, et exposés à l'ignominie, comme il paraît aujourd'hui.
8 “Lakini sasa, kwa muda mfupi, Bwana Mungu wetu amekuwa na neema kwa kutuachia mabaki na kutupa mahali imara katika mahali pake patakatifu, hivyo Mungu wetu atupa mwanga machoni petu na unafuu katika utumwa wetu.
Mais l'Eternel notre Dieu nous a maintenant fait grâce, comme en un moment, de sorte qu'il a fait que quelques-uns [de nous] sont demeurés de reste, et il nous a donné un clou dans son saint lieu, afin que notre Dieu éclairât nos yeux, et nous donnât quelque petit répit dans notre servitude.
9 Ingawa tu watumwa, Mungu wetu hajatuacha katika kufungwa kwetu. Ametuonyesha huruma mbele ya wafalme wa Uajemi: Ametujalia maisha mapya kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wetu na kukarabati magofu yake, naye ametupa ukuta wa ulinzi katika Yuda na Yerusalemu.
Car nous sommes esclaves, et toutefois notre Dieu ne nous a point abandonnés dans notre servitude; mais il nous a fait trouver grâce devant les Rois de Perse, pour nous donner du répit, afin de relever la maison de notre Dieu, et rétablir ses lieux déserts, et pour nous donner une cloison en Juda, et à Jérusalem.
10 “Lakini sasa, Ee Mungu wetu, tunaweza kusema nini baada ya hili? Kwa maana tumedharau maagizo
Mais maintenant, ô notre Dieu! que dirons-nous après ces choses? car nous avons abandonné tes commandements,
11 uliyoyatoa kupitia watumishi wako manabii uliposema: ‘Nchi mnayoiingia kuimiliki ni nchi iliyochafuliwa na uovu wa watu wake. Kwa matendo yao ya machukizo wameijaza nchi kwa unajisi wao kutoka mwisho mmoja hadi mwingine.
Que tu as donnés par tes serviteurs les Prophètes, en disant: Le pays auquel vous allez entrer pour le posséder, est un pays souillé par la souillure des peuples de ces pays-là, à cause des abominations dont ils l'ont rempli, depuis un bout jusqu'à l'autre par leurs impuretés.
12 Kwa hiyo, msiwaoze binti zenu kwa wana wao wala binti zao kwa wana wenu. Msitafute mkataba wa urafiki nao kwa wakati wowote. Ndipo mtakapofanikiwa na kula mema ya nchi na kuwaachia watoto wenu nchi hiyo kama urithi wao wa milele.’
Maintenant donc, ne donnez point vos filles à leurs fils, et ne prenez point leurs filles pour vos fils, et ne cherchez point leur paix, ni leur bien à jamais; afin que vous soyez affermis, et que vous mangiez les biens du pays, et que vous le fassiez hériter à vos fils pour toujours.
13 “Yale yaliyotupata ni matokeo ya matendo yetu mabaya, pia hatia yetu kubwa. Hata hivyo, wewe Mungu wetu, umetuadhibu kidogo kuliko dhambi zetu zilivyostahili na umetupa mabaki kama haya.
Or après toutes les choses qui nous sont arrivées à cause de nos mauvaises œuvres, et du grand crime qui s'est trouvé en nous; [et] parce, ô notre Dieu! que tu es demeuré [dans tes punitions] au dessous de ce que nos péchés [méritaient], et que tu nous as donné un résidu tel qu'est celui-ci;
14 Je, tutavunja maagizo yako tena na kuoana na watu ambao hufanya mambo ya machukizo? Je, hutakuwa na hasira ya kutosha juu yetu na kutuangamiza, bila kutuachia mabaki wala atakayenusurika?
Retournerions-nous à enfreindre tes commandements, et à faire alliance avec ces peuples abominables? Ne serais-tu pas irrité contre nous, jusqu'à nous consumer, en sorte qu'il n'y aurait plus aucun résidu, ni aucune ressource?
15 Ee Bwana, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki! Leo hii tumeachwa kama mabaki. Tupo hapa mbele zako na hatia yetu, ingawa katika hali hii hakuna hata mmoja wetu anayeweza kusimama mbele zako.”
Eternel Dieu d'Israël! tu es juste; car nous sommes demeurés de reste, comme il se [voit] aujourd'hui. Voici, nous sommes devant toi avec notre crime; quoiqu'il n'y ait pas moyen de subsister devant toi à cause de ce [que nous avons fait].

< Ezra 9 >