< Ezra 9 >

1 Baada ya mambo haya kutendeka, viongozi walinijia na kusema, “Watu wa Israeli, wakiwemo makuhani na Walawi, hawakujitenga na majirani zao katika kufanya machukizo, kama yale ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri na Waamori.
Après cela, les chefs vinrent me trouver, et ils me dirent: Le peuple d'Israël, les prêtres, les lévites, ne sont plus séparés des peuples de la terre en leurs abominations; du Chananéen, de l'Hettéen, du Phérézéen, du Jébuséen, de l'Ammonite, du Moabite, du Mosérite, de l'Amorrhéen.
2 Wamewaoa baadhi ya binti zao kuwa wake zao na wake za wana wao, nao wamechanganya taifa takatifu na watu waliowazunguka. Nao viongozi na maafisa wamekuwa mstari wa mbele katika njia hii potovu.”
Ils se sont mariés, eux et leurs fils, parmi ces peuples, et la semence sainte s'est détournée dans les nations de la terre, et la main des princes a été la première, en cette infraction à la loi.
3 Niliposikia jambo hili nilirarua koti langu na joho langu, nikazingʼoa nywele za kichwa changu na ndevu zangu na kuketi nikishangaa.
Or, quand j'ouïs ces paroles, je déchirai mes vêtements, je fus saisi de crainte; je m'arrachai les cheveux et la barbe, et je m'assis tout contristé.
4 Kisha kila mmoja aliyetetemeshwa na maneno ya Mungu wa Israeli alikusanyika kunizunguka kwa sababu ya upotovu huu wa hao watu waliorudi kutoka utumwani. Nami niliketi pale nikishangaa mpaka wakati wa dhabihu ya jioni.
Et tous ceux qui suivaient la loi du Dieu d'Israël s'assemblèrent auprès de moi, à cause de cette infraction aux préceptes; et moi, toujours assis, je gardai un morne silence jusqu'au sacrifice du soir.
5 Ndipo wakati wa kutoa dhabihu ya jioni nikainuka kutoka kujidhili kwangu nikiwa na koti na joho langu lililoraruka, nikapiga magoti mikono yangu ikiwa imeinuliwa kwa Bwana Mungu wangu.
Et pendant le sacrifice du soir, je sortis de mon abattement; après avoir déchiré mes vêtements, saisi de crainte, je me mis à genoux, et j'étendis mes mains vers le Seigneur Dieu.
6 Nami nikaomba: “Ee Mungu wangu, natahayari na kuona aibu kukuinulia uso wangu Mungu wangu, kwa sababu dhambi zetu zimejikusanya hata kupita juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imefika mbinguni.
Et je dis: Seigneur, je suis plein de honte et de confusion, ô mon Dieu, en levant mon front devant vous; car nos dérèglements se sont accumulés sur nos têtes, et nos péchés ont monté jusqu'au ciel.
7 Tokea siku za babu zetu mpaka sasa, hatia yetu imekuwa kubwa. Kwa sababu ya dhambi zetu, sisi na wafalme wetu na makuhani wetu tumekabiliwa na vita, utumwa, kutekwa na kudhiliwa katika mikono ya wafalme wa kigeni, kama ilivyo leo.
Depuis les jours de nos pères jusqu'à ce jour, nous avons vécu dans le péché, et à cause de nos transgressions, nous, nos rois, nos fils, nous avons été livrés aux rois des nations, par le glaive, la captivité, le pillage, et nous avons eu la honte au front comme nous l'avons encore.
8 “Lakini sasa, kwa muda mfupi, Bwana Mungu wetu amekuwa na neema kwa kutuachia mabaki na kutupa mahali imara katika mahali pake patakatifu, hivyo Mungu wetu atupa mwanga machoni petu na unafuu katika utumwa wetu.
Maintenant, notre Dieu a été bienveillant pour nous jusqu'à nous sauver, nous rétablir en ce lieu où est son sanctuaire, nous éclaircir les yeux, et nous accorder un peu de vie dans notre esclavage.
9 Ingawa tu watumwa, Mungu wetu hajatuacha katika kufungwa kwetu. Ametuonyesha huruma mbele ya wafalme wa Uajemi: Ametujalia maisha mapya kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wetu na kukarabati magofu yake, naye ametupa ukuta wa ulinzi katika Yuda na Yerusalemu.
Car nous sommes esclaves; toutefois, en notre servitude, le Seigneur notre Dieu ne nous a pas abandonnés, et il nous a fait trouver miséricorde devant les rois de Perse, pour qu'ils nous accordassent un peu de vie, qu'ils relevassent le temple de notre Dieu, qu'ils le rétablissent en sa désolation, et qu'ils nous rendissent plus de sûreté en Juda et à Jérusalem.
10 “Lakini sasa, Ee Mungu wetu, tunaweza kusema nini baada ya hili? Kwa maana tumedharau maagizo
Que dirons-nous après cela, ô notre Dieu? Car nous avons abandonné vos commandements,
11 uliyoyatoa kupitia watumishi wako manabii uliposema: ‘Nchi mnayoiingia kuimiliki ni nchi iliyochafuliwa na uovu wa watu wake. Kwa matendo yao ya machukizo wameijaza nchi kwa unajisi wao kutoka mwisho mmoja hadi mwingine.
Que vous nous aviez donnés par vos serviteurs les prophètes, disant: La terre où vous allez pour qu'elle soit votre héritage est une terre troublée de fond en comble par les abominations des peuples qui l'habitent, et qui l'ont remplie d'un bout à l'autre de leurs impuretés.
12 Kwa hiyo, msiwaoze binti zenu kwa wana wao wala binti zao kwa wana wenu. Msitafute mkataba wa urafiki nao kwa wakati wowote. Ndipo mtakapofanikiwa na kula mema ya nchi na kuwaachia watoto wenu nchi hiyo kama urithi wao wa milele.’
Ne donnez donc pas vos filles à leurs fils, et ne prenez point pour vos fils leurs filles; ne cherchez jamais leur pain ni leur bien-être, afin que vous vous affermissiez, que vous mangiez les biens de cette terre, et que vous les transmettiez en héritage à vos fils pour toujours.
13 “Yale yaliyotupata ni matokeo ya matendo yetu mabaya, pia hatia yetu kubwa. Hata hivyo, wewe Mungu wetu, umetuadhibu kidogo kuliko dhambi zetu zilivyostahili na umetupa mabaki kama haya.
Or, après tout ce qui nous est advenu à cause de nos mauvaises actions et de nos grands péchés, vous nous avez sauvés, parce qu'il n'est point de Dieu tel que vous, et que vous avez ôté nos iniquités.
14 Je, tutavunja maagizo yako tena na kuoana na watu ambao hufanya mambo ya machukizo? Je, hutakuwa na hasira ya kutosha juu yetu na kutuangamiza, bila kutuachia mabaki wala atakayenusurika?
Et nous avons recommencé à répudier vos commandements, à nous marier parmi ces peuples; ô Seigneur, ne soyez pas irrité contre nous jusqu'à nous anéantir, sans que nul parmi nous échappe et soit épargné.
15 Ee Bwana, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki! Leo hii tumeachwa kama mabaki. Tupo hapa mbele zako na hatia yetu, ingawa katika hali hii hakuna hata mmoja wetu anayeweza kusimama mbele zako.”
Seigneur Dieu d'Israël, vous êtes juste, car nous voilà sains et saufs en ce jour; voilà que nous sommes devant vous dans nos péchés, et après de tels excès on ne peut subsister devant vous.

< Ezra 9 >