< Ezra 9 >

1 Baada ya mambo haya kutendeka, viongozi walinijia na kusema, “Watu wa Israeli, wakiwemo makuhani na Walawi, hawakujitenga na majirani zao katika kufanya machukizo, kama yale ya Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri na Waamori.
Forsothe after that these thingis weren fillid, the princes neiyeden to me, and seiden, The puple of Israel, and the prestis, and dekenes, ben not depertid fro the `puplis of londis, and fro abhominaciouns of hem, that is, of Cananei, of Ethei, and of Pheresei, and of Jebusei, and of Amonytis, and of Moabitis, and of Egipcians, and of Ammorreis.
2 Wamewaoa baadhi ya binti zao kuwa wake zao na wake za wana wao, nao wamechanganya taifa takatifu na watu waliowazunguka. Nao viongozi na maafisa wamekuwa mstari wa mbele katika njia hii potovu.”
For thei han take `of her douytris wyues to hem silf, and to her sones, and thei han medlid hooli seed with the puplis of londis; also the hond of princes and of magistratis was the firste in this trespassyng.
3 Niliposikia jambo hili nilirarua koti langu na joho langu, nikazingʼoa nywele za kichwa changu na ndevu zangu na kuketi nikishangaa.
And whanne Y hadde herd this word, Y torente my mentil and coote, and Y pullide awei the heeris of myn heed and berd, and Y sat morenynge.
4 Kisha kila mmoja aliyetetemeshwa na maneno ya Mungu wa Israeli alikusanyika kunizunguka kwa sababu ya upotovu huu wa hao watu waliorudi kutoka utumwani. Nami niliketi pale nikishangaa mpaka wakati wa dhabihu ya jioni.
Forsothe alle that dredden the word of God of Israel camen togidere to me, for the trespassyng of hem that weren comun fro caitifte; and Y sat sori `til to the sacrifice of euentid.
5 Ndipo wakati wa kutoa dhabihu ya jioni nikainuka kutoka kujidhili kwangu nikiwa na koti na joho langu lililoraruka, nikapiga magoti mikono yangu ikiwa imeinuliwa kwa Bwana Mungu wangu.
And in the sacrifice of euentid Y roos fro myn afflicioun, and aftir that Y to-rente the mentil and coote, Y bowide my knees, and I spredde abrood myn hondis to `my Lord God,
6 Nami nikaomba: “Ee Mungu wangu, natahayari na kuona aibu kukuinulia uso wangu Mungu wangu, kwa sababu dhambi zetu zimejikusanya hata kupita juu ya vichwa vyetu na hatia yetu imefika mbinguni.
and Y seide, My God, Y am confoundid and aschamed to reise my face to thee, for oure wickidnessis ben multiplied `on myn heed, and oure trespassis encreessiden `til to heuene,
7 Tokea siku za babu zetu mpaka sasa, hatia yetu imekuwa kubwa. Kwa sababu ya dhambi zetu, sisi na wafalme wetu na makuhani wetu tumekabiliwa na vita, utumwa, kutekwa na kudhiliwa katika mikono ya wafalme wa kigeni, kama ilivyo leo.
fro the daies of oure fadris; but also we vs silf han synned greuousli `til to this dai, and for our wickidnessis we, and oure kyngis, and oure prestis ben bitakun in the hondis of kyngis of londis, bothe in to swerd, and in to caitifte, in to raueyn, and in to schenship of cheer, as also in this dai.
8 “Lakini sasa, kwa muda mfupi, Bwana Mungu wetu amekuwa na neema kwa kutuachia mabaki na kutupa mahali imara katika mahali pake patakatifu, hivyo Mungu wetu atupa mwanga machoni petu na unafuu katika utumwa wetu.
And now as at a litil and at a moment oure preier is maad anentis `oure Lord God, that relikis schulden be left to vs, and that `his pees schulde be youun in his hooli place, and that oure God schulde liytne oure iyen, and yyue to vs a litil lijf in oure seruage.
9 Ingawa tu watumwa, Mungu wetu hajatuacha katika kufungwa kwetu. Ametuonyesha huruma mbele ya wafalme wa Uajemi: Ametujalia maisha mapya kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wetu na kukarabati magofu yake, naye ametupa ukuta wa ulinzi katika Yuda na Yerusalemu.
For we ben seruauntis, and oure God forsoke vs not in oure seruage; and he bowide merci on vs bifor the king of Persis, that he schulde yyue lijf to vs, and enhaunse the hows of oure God, and that he schulde bilde the wildernessis therof, and yyue to vs hope in Juda and in Jerusalem.
10 “Lakini sasa, Ee Mungu wetu, tunaweza kusema nini baada ya hili? Kwa maana tumedharau maagizo
And now, `oure Lord God, what schulen we seie after these thingis? For we han forsake thi comaundementis,
11 uliyoyatoa kupitia watumishi wako manabii uliposema: ‘Nchi mnayoiingia kuimiliki ni nchi iliyochafuliwa na uovu wa watu wake. Kwa matendo yao ya machukizo wameijaza nchi kwa unajisi wao kutoka mwisho mmoja hadi mwingine.
whiche thou comaundidist in the hond of thi seruauntis profetis, and seidist, The lond, to which ye schulen entre, to holde it in possessioun, is an vnclene lond, bi the vnclennesse of puplis, and of othere londis, in the abhomynaciouns of hem, that filliden it with her defoulyng, fro the mouth `til to the mouth.
12 Kwa hiyo, msiwaoze binti zenu kwa wana wao wala binti zao kwa wana wenu. Msitafute mkataba wa urafiki nao kwa wakati wowote. Ndipo mtakapofanikiwa na kula mema ya nchi na kuwaachia watoto wenu nchi hiyo kama urithi wao wa milele.’
Now therfor yiue ye not youre douytris to her sones, and take ye not her douytris to youre sones; and seke ye not the pees of hem and the prosperite `of hem `til in to with outen ende; that ye be coumfortid, and ete the goodis, that ben of the lond, and that ye haue eiris, youre sones, `til in to `the world.
13 “Yale yaliyotupata ni matokeo ya matendo yetu mabaya, pia hatia yetu kubwa. Hata hivyo, wewe Mungu wetu, umetuadhibu kidogo kuliko dhambi zetu zilivyostahili na umetupa mabaki kama haya.
And after alle thingis that camen on vs in oure werste werkis, and in oure grete trespas, for thou, oure God, hast delyuered vs fro oure wickidnesse, and hast youe helthe to vs,
14 Je, tutavunja maagizo yako tena na kuoana na watu ambao hufanya mambo ya machukizo? Je, hutakuwa na hasira ya kutosha juu yetu na kutuangamiza, bila kutuachia mabaki wala atakayenusurika?
as `it is to dai, that we schulden not be turned, and make voide thi comaundementis, and that we schulden not ioyne matrimonyes with the puplis of these abhomynacouns. Whether thou art wrooth to vs `til to the endyng, that thou schuldist not leeue to us remenauntis, and helthe?
15 Ee Bwana, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki! Leo hii tumeachwa kama mabaki. Tupo hapa mbele zako na hatia yetu, ingawa katika hali hii hakuna hata mmoja wetu anayeweza kusimama mbele zako.”
Lord God of Israel, thou art iust; for we ben left, that schulden be sauyd as in this day, lo! we ben bifor thee in oure synne; for me may `not stonde bifor thee on this thing.

< Ezra 9 >