< Ezra 8 >
1 Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
Now estes são os chefes de família de seus pais, e esta é a genealogia daqueles que subiram comigo da Babilônia, no reinado de Artaxerxes, o rei:
2 wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
Dos filhos de Phinehas, Gershom. Dos filhos de Ithamar, Daniel. Dos filhos de David, Hattush.
3 wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
Dos filhos de Shecaniah, dos filhos de Parosh, Zacarias; e com ele foram listados por genealogia dos homens cento e cinqüenta.
4 wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
Dos filhos de Pahathmoab, Eliehoenai o filho de Zerahiah; e com ele duzentos homens.
5 wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
Dos filhos de Shecaniah, o filho de Jahaziel; e com ele trezentos homens.
6 wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
Dos filhos de Adin, Ebed o filho de Jonathan; e com ele cinqüenta homens.
7 wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
Dos filhos de Elão, Jesaías o filho de Atalia; e com ele setenta homens.
8 wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
Dos filhos de Shephatiah, Zebadiah o filho de Michael; e com ele oitenta homens.
9 wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
Dos filhos de Joab, Obadiah o filho de Jehiel; e com ele duzentos e dezoito homens.
10 wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
Dos filhos de Shelomith, o filho de Josiphiah; e com ele cento e sessenta homens.
11 wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
Dos filhos de Bebai, Zacarias o filho de Bebai; e com ele vinte e oito homens.
12 wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
Dos filhos de Azgad, Johanan o filho de Hakkatan; e com ele cento e dez homens.
13 wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
Dos filhos de Adonikam, que foram os últimos, seus nomes são: Eliphelet, Jeuel e Semaías; e com eles sessenta homens.
14 wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
Dos filhos de Bigvai, Uthai e Zabbud; e com eles setenta homens.
15 Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
Eu os reuni no rio que corre para o Ahava; e lá ficamos acampados três dias. Depois olhei em volta para o povo e para os sacerdotes, e descobri que não havia nenhum dos filhos de Levi.
16 Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
Então mandei buscar Eliezer, Ariel, Semaías, Elnatã, Jaribe, Elnatã, Nathan, Zacarias e Meshullam, chefes; também Joiaribe e Elnatã, que eram professores.
17 nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
Enviei-os à Iddo, o chefe do lugar Casiphia; e lhes disse o que deveriam dizer à Iddo e seus irmãos, os servos do templo no lugar Casiphia, que deveriam trazer-nos ministros para a casa de nosso Deus.
18 Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
De acordo com a boa mão do nosso Deus sobre nós, eles nos trouxeram um homem de discrição, dos filhos de Mali, filho de Levi, filho de Israel, ou seja, Serebias, com seus filhos e seus irmãos, dezoito;
19 Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
e Hasabias, e com ele Jesaías dos filhos de Merari, seus irmãos e seus filhos, vinte;
20 Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
e dos servos do templo, que Davi e os príncipes tinham dado para o serviço dos levitas, duzentos e vinte servos do templo. Todos eles foram mencionados pelo nome.
21 Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
Então proclamei um jejum lá no rio Ahava, para que nos humilhássemos diante de nosso Deus, para buscar dele um caminho reto para nós, para nossos pequenos e para todos os nossos bens.
22 Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
Pois tive vergonha de pedir ao rei um bando de soldados e cavaleiros para nos ajudar contra o inimigo no caminho, porque tínhamos falado com o rei, dizendo: “A mão de nosso Deus está sobre todos aqueles que o buscam, para o bem; mas seu poder e sua ira estão contra todos aqueles que o abandonam”.
23 Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
Portanto, jejuamos e imploramos a nosso Deus por isso, e ele atendeu nosso pedido.
24 Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
Então separei doze dos chefes dos sacerdotes, até mesmo Serebias, Hasabias e dez de seus irmãos com eles,
25 nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
e pesei-lhes a prata, o ouro e os vasos, até mesmo a oferta pela casa de nosso Deus, que o rei, seus conselheiros, seus príncipes e todo o Israel ali presente, haviam oferecido.
26 Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
pesei na mão deles seiscentos e cinqüenta talentos de prata, cem talentos de vasos de prata, cem talentos de ouro,
27 mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
vinte taças de ouro pesando mil dracmas, e dois vasos de bronze fino e brilhante, preciosos como o ouro.
28 Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
Eu lhes disse: “Vocês são santos para Yahweh, e os vasos são santos. A prata e o ouro são uma oferta de livre vontade a Iavé, o Deus de seus pais”.
29 Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
Vigie-os e guarde-os até pesá-los diante dos chefes dos sacerdotes, dos levitas e dos príncipes das casas dos pais de Israel em Jerusalém, nos quartos da casa de Iavé”.
30 Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
Assim, os sacerdotes e os levitas receberam o peso da prata, do ouro e dos vasos, para levá-los a Jerusalém para a casa de nosso Deus.
31 Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
Então partimos do rio Ahava no décimo segundo dia do primeiro mês, para ir a Jerusalém. A mão de nosso Deus estava sobre nós, e ele nos livrou da mão do inimigo e dos bandidos, a propósito.
32 Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
Viemos a Jerusalém, e lá ficamos três dias.
33 Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
No quarto dia a prata, o ouro e os vasos foram pesados na casa de nosso Deus na mão de Meremoth, filho de Uriah, o sacerdote; e com ele Eleazar, filho de Finéias; e com eles Jozabad, filho de Jeshua, e Noadiah, filho de Binnui, os levitas.
34 Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
Tudo foi contado e pesado; e todo o peso foi escrito naquela época.
35 Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
As crianças do cativeiro, que haviam saído do exílio, ofereceram holocaustos ao Deus de Israel: doze touros para todo Israel, noventa e seis carneiros, setenta e sete cordeiros e doze bodes para uma oferta pelo pecado. Tudo isso era um holocausto para Iavé.
36 Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.
Eles entregaram as comissões do rei para os governadores locais do rei e para os governadores além do rio. Então eles apoiaram o povo e a casa de Deus.