< Ezra 8 >
1 Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
Or ce sont ici les Chefs des pères, avec le dénombrement qui fut fait selon les généalogies, de ceux qui montèrent avec moi de Babylone, pendant le règne du Roi Artaxerxes;
2 wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
Des enfants de Phinées, Guersom; des enfants d'Ithamar, Daniel; des enfants de David, Hattus;
3 wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
Des enfants de Sécania, qui était des enfants de Parhos, Zacharie, et avec lui, en faisant le dénombrement par leur généalogie selon les mâles, cent cinquante hommes.
4 wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
Des enfants de Péhath-Moab, Eliehohénaï fils de Zérahia, et avec lui deux cents hommes;
5 wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
Des enfants de Sécania, le fils de Jahaziël, et avec lui trois cents hommes;
6 wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
Des enfants de Hadin, Hébed fils de Jonathan, et avec lui cinquante hommes;
7 wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
Des enfants de Hélam, Esaïe, fils de Hathalia, et avec lui soixante-dix hommes;
8 wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
Des enfants de Sépharia, Zébadia fils de Micaël, et avec lui quatre-vingts hommes;
9 wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
Des enfants de Joab, Habadia fils de Jéhiël, et avec lui deux cent dix-huit hommes;
10 wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
Des enfants de Sélomith, le fils de Josiphia, et avec lui cent soixante hommes;
11 wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
Des enfants de Bébaï, Zacharie fils de Bébaï, et avec lui vingt-huit hommes;
12 wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
Des enfants de Hazgad, Johanan, fils de Katan, et avec lui cent et dix hommes;
13 wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
Des enfants d'Adonicam, les derniers, desquels les noms sont Eliphelet, Jéhiël, et Sémahia, et avec eux soixante hommes.
14 wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
Des enfants de Bigvaï, Huthaï, Zabbud, et avec eux soixante-dix hommes.
15 Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
Et je les assemblai près de la rivière, qui se rend à Ahava, et nous y demeurâmes trois jours. Puis je pris garde au peuple et aux Sacrificateurs, et je n'y trouvai aucun des enfants de Lévi.
16 Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
Et ainsi j'envoyai d'entre les principaux Elihéser, Ariel, Sémahia, Elnathan, Jarib, Elnathan, Nathan, Zacharie, et Mésullam, avec Jojarib et Elnathan, docteurs.
17 nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
Et je leur donnai des ordres pour Iddo, principal chef, [qui demeurait] dans le lieu de Casiphia; et je mis en leur bouche les paroles qu'ils devaient dire à Iddo, [et] à son frère, Néthiniens, dans le lieu de Casiphia, afin qu'ils nous fissent venir des ministres pour la maison de notre Dieu.
18 Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
Et ils nous amenèrent, selon que la main de notre Dieu était bonne sur nous, un homme intelligent, d'entre les enfants de Mahli, fils de Lévi, fils d'Israël; [savoir] Sérébia, avec ses fils et ses frères, [qui furent] dix-huit hommes.
19 Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
Et Hasabia, et avec lui Esaïe, d'entre les enfants de Mérari, ses frères, et leurs enfants, vingt hommes.
20 Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
Et des Néthiniens, que David et les principaux du peuple avaient assignés pour le service des Lévites, deux cent et vingt Néthiniens, qui furent tous nommés par leurs noms.
21 Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
Et je publiai là le jeûne auprès de la rivière d'Ahava, afin de nous humilier devant notre Dieu, le priant de nous donner un heureux voyage pour nous, et pour nos familles, et pour tous nos biens.
22 Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
Car j'eus honte de demander au Roi des forces et des gens de cheval pour nous défendre des ennemis par le chemin; à cause que nous avions dit au Roi en termes exprès: La main de notre Dieu est favorable à tous ceux qui l'invoquent; mais sa force et sa colère est contre ceux qui l'abandonnent.
23 Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
Nous jeûnâmes donc, et nous implorâmes [le secours] de notre Dieu à cause de cela; et il fut fléchi par nos prières.
24 Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
Alors je séparai douze des principaux des Sacrificateurs; avec Sérébia, Hasabia, et avec eux dix de leurs frères.
25 nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
Et je leur pesai l'argent et l'or et les ustensiles, qui étaient l'offrande que le Roi, ses conseillers, ses gentilshommes, et tous ceux d'Israël qui s'[y] étaient trouvés, avaient faite à la maison de notre Dieu.
26 Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
Je leur pesai donc, et je leur délivrai six cent cinquante talents d'argent, et des plats d'argent [pesant] cent talents, et cent talents d'or.
27 mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
Et vingt plats d'or [montant] à mille drachmes, et deux ustensiles de cuivre resplendissant et fin, aussi précieux que s'ils eussent été d'or.
28 Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
Et je leur dis: Vous êtes sanctifiés à l'Eternel; et les ustensiles sont sanctifiés; et cet argent et cet or est une offrande volontaire faite à l'Eternel le Dieu de vos pères.
29 Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
Ayez-y l'œil et gardez-les, jusqu'à ce que vous les pesiez en la présence des principaux des Sacrificateurs et des Lévites, et devant les principaux des pères d'Israël à Jérusalem, dans les chambres de la maison de l'Eternel.
30 Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
Les Sacrificateurs donc et les Lévites reçurent le poids de l'argent, et de l'or, et des ustensiles, pour les apporter à Jérusalem, dans la maison de notre Dieu.
31 Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
Et nous partîmes de la rivière d'Ahava le douzième jour du premier mois, pour aller à Jérusalem; et la main de notre Dieu fut sur nous; et il nous délivra de la main des ennemis, et de [leurs] embûches sur le chemin.
32 Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
Puis nous arrivâmes à Jérusalem, et nous étant reposés trois jours,
33 Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
Au quatrième jour nous pesâmes l'argent et l'or, et les ustensiles dans la maison de notre Dieu, et nous les délivrâmes à Mérémoth, fils d'Urija Sacrificateur, avec lequel [était] Eléazar fils de Phinées; et avec eux Jozabad fils de Jésuah, et Nohadia, fils de Binuï, Lévites.
34 Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
Selon le nombre et le poids de toutes ces choses, et tout le poids en fut mis alors par écrit.
35 Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
Et ceux qui avaient été transportés, [et] qui étaient retournés de la captivité, offrirent pour tout Israël, en holocauste au Dieu d'Israël, douze veaux, quatre-vingt-seize béliers, soixante-dix-sept agneaux, [et] douze boucs pour le péché; le tout en holocauste à l'Eternel.
36 Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.
Et ils remirent les ordonnances du Roi entre les mains des Satrapes du Roi et des Gouverneurs qui étaient au deçà du fleuve, lesquels favorisèrent le peuple, et la maison de Dieu.