< Ezra 8 >
1 Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
Voici les chefs de famille — avec leur généalogie, — de ceux qui montèrent avec moi de Babylone, sous le règne du roi Artaxerxès.
2 wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
Des fils de Phinées, Gersom; des fils d’Ithamar, Daniel; des fils de David, Hattus,
3 wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
qui descendait de Séchénias; des fils de Pharos, Zacharie, et avec lui cent cinquante mâles inscrits dans le registre de famille.
4 wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
Des fils de Phahath-Moab, Elioénaï, fils de Zaréhias, et avec lui deux cents mâles;
5 wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
des fils de Séchénias, fils d’Ezéchiel, et avec lui trois cents mâles;
6 wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
des fils d’Adin, Abed, fils de Jonathan, et avec lui cinquante mâles;
7 wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
des fils d’Elam, Isaïe, fils d’Athalias, et avec lui soixante-dix mâles;
8 wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
des fils de Saphatias, Zébédias, fils de Michaël, et avec lui quatre-vingts mâles;
9 wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
des fils de Joab, Obédias, fils de Jéhiel, et avec lui deux cent dix-huit mâles;
10 wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
des fils de Selomith, fils de Joséphias, et avec lui cent soixante mâles;
11 wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
des fils de Bébaï, Zacharie, fils de Bébaï, et avec lui vingt-huit mâles;
12 wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
des fils d’Azgad, Johanan, fils d’Eccétan, et avec lui cent dix mâles;
13 wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
des fils d’Adonicam, les derniers, dont voici les noms: Eliphélet, Jéhiel et Samaïas, et avec eux soixante mâles;
14 wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
des fils de Béguaï, Uthaï et Zachur, et avec eux soixante-dix mâles.
15 Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
Je les rassemblai près de la rivière qui coule vers Ahava, et nous campâmes là trois jours. Ayant porté mon attention sur le peuple et sur les prêtres, je ne trouvai là aucun des fils de Lévi.
16 Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
Alors je fis appeler les chefs Eliézer, Ariel, Séméïas, Elnathan, Jarib, un autre Elnathan, Nathan, Zacharie et Mosollam, ainsi que les docteurs Joïarib et Elnathan.
17 nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
Je les envoyai vers le chef Eddo, à l’endroit appelé Chasphia, et je mis dans leur bouche les paroles qu’ils devaient dire à Eddo et à ses frères les Nathinéens qui étaient à l’endroit appelé Chasphia, afin qu’ils nous amenassent des ministres pour la maison de notre Dieu.
18 Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
Et comme la main bienfaisante de notre Dieu était sur nous, ils nous amenèrent un homme intelligent, d’entre les fils de Moholi, fils de Lévi, fils d’Israël, savoir Sarabias, et avec lui ses fils et ses frères au nombre de dix-huit;
19 Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
Hasabias, et avec lui Isaïe, d’entre les fils de Mérari,
20 Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
ses frères et leurs fils au nombre de vingt; et d’entre les Nathinéens, que David et les chefs avaient donnés pour le service des lévites, deux cent vingt Nathinéens, tous nominativement désignés.
21 Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
Je publiai là, près de la rivière d’Ahava, un jeûne pour nous affliger devant notre Dieu, afin d’implorer de lui un heureux voyage pour nous, pour nos enfants et pour tout ce qui nous appartenait.
22 Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
Car j’aurais eu honte de demander au roi une escorte et des cavaliers pour nous secourir contre l’ennemi pendant la route, parce que nous avions dit au roi: « La main de notre Dieu est pour leur bien sur tous ceux qui le cherchent, mais sa force et sa colère sont sur tous ceux qui l’abandonnent. »
23 Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
Et à cause de cela nous jeûnâmes et nous invoquâmes notre Dieu; et il nous exauça.
24 Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
Je choisis douze chefs des prêtres, Sarabias et Hasabias, et dix de leurs frères.
25 nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
Je pesai devant eux l’argent, l’or et les ustensiles, offrande qu’avaient prélevée pour la maison de notre Dieu le roi, ses conseillers et ses chefs, et tous ceux d’Israël qui se trouvaient là;
26 Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
et je pesai, en les remettant entre leurs mains, six cent cinquante talents d’argent, des ustensiles d’argent de la valeur de cent talents, cent talents d’or,
27 mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
vingt coupes d’or de la valeur de mille dariques, et deux vases d’un bel airain brillant, aussi précieux que l’or.
28 Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
Et je leur dis: « Vous êtes saints devant Yahweh, et ces ustensiles sont saints, cet argent et cet or sont une offrande volontaire à Yahweh, Dieu de vos pères.
29 Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
Soyez vigilants à les garder, jusqu’à ce que vous les pesiez devant les chefs des prêtres et des lévites, et devant les chefs de famille d’Israël, à Jérusalem, dans les chambres de la maison de Yahweh. »
30 Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
Et les prêtres et les lévites reçurent au poids l’argent, l’or et les ustensiles, pour les porter à Jérusalem dans la maison de notre Dieu.
31 Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
Nous partîmes de la rivière d’Ahava le douzième jour du premier mois, pour nous rendre à Jérusalem. La main de notre Dieu fut sur nous, et nous sauva des mains de l’ennemi et des embûches pendant la route.
32 Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
Arrivés à Jérusalem, nous nous y reposâmes trois jours.
33 Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
Le quatrième jour, l’argent, l’or et les ustensiles furent pesés, dans la maison de notre Dieu, entre les mains de Mérimuth, fils d’Urie, le prêtre; il y avait avec lui Eléazar, fils de Phinées et avec eux les lévites Jozabad, fils de Josué, et Noadias, fils de Bennui.
34 Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
Le tout fut livré selon le nombre et selon le poids; et le poids total fut mis par écrit en ce temps-là.
35 Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
Ceux qui revenaient de l’exil, les fils de la captivité, offrirent en holocauste au Dieu d’Israël douze taureaux pour tout Israël, quatre-vingt-seize béliers, soixante-dix-sept agneaux, douze boucs pour le péché, le tout en holocauste à Yahweh.
36 Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.
Ils transmirent les ordres du roi aux satrapes du roi et aux gouverneurs d’au delà du fleuve, et ceux-ci soutinrent le peuple et la maison de Dieu.