< Ezra 7 >
1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
Bu olaylardan sonra, Pers Kralı Artahşasta'nın krallığı döneminde, Başkâhin Harun oğlu Elazar oğlu Pinehas oğlu Avişua oğlu Bukki oğlu Uzzi oğlu Zerahya oğlu Merayot oğlu Azarya oğlu Amarya oğlu Ahituv oğlu Sadok oğlu Şallum oğlu Hilkiya oğlu Azarya oğlu Seraya oğlu Ezra adında biri Babil'den geldi. Ezra İsrail'in Tanrısı RAB'bin Musa'ya verdiği yasayı iyi bilen bir bilgindi. Tanrısı RAB'bin yardımıyla kral ona her istediğini verdi.
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
7 Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
Kral Artahşasta'nın krallığının yedinci yılında İsrail halkından, kâhinlerden, Levililer'den, ezgicilerden, tapınak görevlilerinden ve kapı nöbetçilerinden bazıları Yeruşalim'e gitti.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
Ezra, Artahşasta'nın krallığının yedinci yılının beşinci ayında Yeruşalim'e vardı.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
Birinci ayın birinci günü Babil'den ayrılmıştı. Tanrısı'nın koruyucu eli sayesinde beşinci ayın birinci günü Yeruşalim'e vardı.
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
Ezra kendini RAB'bin Yasası'nı inceleyip uygulamaya ve İsrail'de kuralları, ilkeleri öğretmeye adamıştı.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
Kral Artahşasta'nın RAB'bin buyruklarını, İsrail için koyduğu kuralları iyi bilen Kâhin ve Bilgin Ezra'ya verdiği mektubun bir örneği şudur:
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
“Kralların Kralı Artahşasta'dan Gökler Tanrısı'nın Yasası'nın bilgini Kâhin Ezra'ya selamlar!
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
“Krallığımda yaşayan İsrail halkından, kâhinlerden ve Levililer'den Yeruşalim'e gitmek isteyen herkesin seninle gidebilmesi için buyruk veriyorum.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
Elindeki Tanrın'ın Yasası'nın uygulanıp uygulanmadığı konusunda Yahuda ve Yeruşalim'de araştırma yapman için, ben ve yedi danışmanım seni görevlendirdik.
15 Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
Benim ve danışmanlarımın Yeruşalim'de konut kuran İsrail'in Tanrısı'na gönülden verdiğimiz altını, gümüşü birlikte götürmelisin.
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
Babil İli'nden elde edeceğin altının, gümüşün tümünü, halkın ve kâhinlerin Tanrıları'nın Yeruşalim'deki Tapınağı'na gönülden verdikleri armağanları da alıp götürmelisin.
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
“Bu parayla hemen boğalar, koçlar, kuzular, tahıl sunuları ve dökmelik sunular satın alacak ve hepsini Tanrın'ın Yeruşalim'deki Tapınağı'nın sunağı üzerinde sunacaksın.
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
Sen ve kardeşlerin artan altını, gümüşü Tanrınız'ın isteği uyarınca dilediğiniz gibi kullanın.
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
Tanrın'ın Tapınağı'nın hizmetinde kullanılmak üzere sana verilen kapların hepsini Yeruşalim'in Tanrısı'na sun.
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
Tanrın'ın Tapınağı için ödemen gereken başka bir şey varsa, giderleri kralın hazinesinden karşılarsın.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
“Ben, Kral Artahşasta, Fırat'ın batı yakasındaki bölgenin bütün hazine görevlilerine buyruk veriyorum: Gökler Tanrısı'nın Yasası'nın bilgini Kâhin Ezra'nın sizden her istediğini özenle yerine getirin.
22 talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
Kendisine gerektiğinde yüz talanta kadar gümüş, yüz kor buğday, yüz bat şarap, yüz bat zeytinyağı ve istediği kadar tuz sağlayın.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
Göklerin Tanrısı kendi tapınağı için ne buyurursa, özenle yerine getirin. Öyle ki, bana ve oğullarıma öfkelenmesin.
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
Şunu da bilesiniz ki, kâhinlerden, Levililer'den, ezgicilerden, tapınak görevlilerinden ve kapı nöbetçilerinden, Tanrı'nın Tapınağı'nın öbür hizmetkârlarından vergi almaya yetkiniz yoktur.
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
“Sana gelince, Ezra, sendeki Tanrı bilgeliği uyarınca yargıçlar ata. Bunlar Fırat'ın batı yakasındaki bölgede yaşayan bütün halka, Tanrın'ın yasalarını bilenlerin hepsine adalet sağlasınlar. Yasayı bilmeyenlere de siz öğreteceksiniz.
26 Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
Tanrın'ın Yasası'na ve kralın buyruklarına uymayanlar ya ölümle, ya sürgünle, ya mallarına el konarak, ya da hapsedilerek cezalandırılsın.”
27 Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
Atalarımızın Tanrısı RAB'be övgüler olsun! Kralın yüreğine Yeruşalim'deki tapınağını onurlandırma isteğini koydu.
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
Kralın, danışmanlarının, güçlü komutanlarının bana iyi davranmalarını sağladı. Tanrım RAB'bin eli üzerimde olduğundan yüreklendim. İsrail ileri gelenlerinin bazılarını toplayıp benimle Yeruşalim'e dönmelerini sağladım.